Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tazama: Jengo laporomoka kutokana na mafuriko China
Mamlaka ya China imeonya kuhusu "majanga mengi " mwezi ujao, huku mvua kubwa ikinyesha katika maeneo ya nchi.
Tahadhari ya hali ya hewa imetolewa kwa maeneo makubwa ya kati na kusini magharibi mwa China na maelfu ya watu wamehamishwa.
Jengo liliporomoka na mafuriko huko Chongqing. Wakati huohuo, katika jimbo la Henan, waokoaji walirekodiwa wakiwaokoa watu waliokuwa wamenaswa juu ya gari katikati ya mkondo wa maji.