Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
‘Zama Zama: Wahamiaji wanaotafuta riziki kwa njia hatari kwenye migodi Afrika Kusini
BBC Africa Eye inakutana na wahamiaji ambao wanahatarisha kila kitu kwenda chini ya ardhi katika machimbo ya dhahabu yaliyotelekezwa nchini Afrika Kusini.
Kila siku wanaenda kazini, hawajui kama watarudi nyumbani wakiwa hai.
Umaskini unawalazimisha chini ya ardhi kutafuta dhahabu. Wengine watakamatwa kwa uchimbaji haramu wa madini.
Wengine watakufa lakini wanalazimika kufanya kazi hii ili kujikimu kimaisha.