Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kemikali za sumu zinavyoathiri wachimba madini Tanzania
Kwa mujibu wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), wakati uchimbaji madini unaajiri karibu 1% ya nguvu kazi duniani, sekta hiyo inasababisha 8% ya ajali zinazoleta vifo.
Hata hivyo watu wengi wanapata madhara ya kiafya ya muda mrefu kutokana na kazi yao ya uchimbaji madini katika maisha yao ya baadaye wakati mwingine hurithisha hadi kwa vizazi vijavyo.
Dayo Yusuf alitembelea mgodi wa dhahabu Kusini Magharibi mwa Tanzania ambapo wachimbaji wadogo hukimbilia dhahabu licha ya hatari kwa afya zao.