Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mabadiliko ya tabia nchi yalivyotenganisha familia
Feroza anamlea mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka sita peke yake. Mume wake alikuwa mkulima lakini alilazimika kuondoka kwenda mjini kwani maji ya chumvi yaliharibu ardhi yao.
Wanaishi katika msitu mkubwa zaidi wa mikoko duniani - Sunderbans -- nchini India. Lakini maji yanaongezeka na visiwa vinazama, kwani vimbunga vinapiga mara kwa mara.