Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Shambulio la 9/11: Dakika 102 zilizobadilisha Marekani na ulimwengu
Mnamo Septemba 11 mwaka 2001 Marekani ilishambuliwa.
Mtandao wenye msimamo mkali wa Kiislamu, al-Qaeda, uliteka nyara ndege nne na kuzitumia kama makombora dhidi ya maeneo maalumu ya Marekani.
Karibu watu 3,000 waliuawa. Marekani ilijibu janga hilo kupitia oparesheni iliyoitwa ‘vita dhidi ya ugaidi’ – iliyojumuisha uvamizi wa nchi mbili na kusabisha vifo zaidi.
Hivi ndivyo mambo yalivyokuwa asubuhi hiyo iliyobadilisha Marekani na ulimwengu.