Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kenya: Wakazi wa Turkana walalamikia kutonufaika na mafuta
Kampuni ya Tullow ilipogundua mafuta kusini mwa bonde la Lokichar mwaka 2012, wenyeji walidhani kwamba eneo hilo lililotengwa hatimaye litaanza kustawi.
Inasemekana kwamba bonde hilo lina uwezo wa kutoa mapipa milioni 560 ya mafuta katika vyanzo ilivyo navyo. Lakini miaka saba baadaye, wenyeji bado hawajapata manufaa ya kuridhisha.
Hivi karibuni Rais Kenyatta alizindua shehena ya bareli 240,000 ambayo iliuzwa kwa dola milioni 12.
Wenyeji wa eneo la Lokitoeliwo lililopatikana mafuta, walilitumia kulisha mifugo lakini kwa sasa linatumika kwa uchimbaji wa bidhaa hiyo kwenye visima vya eneo la Ngamia ambalo wanadai kukumbana na ukosefu wa maji, umaskini na njaa.