BBC Africa Eye: Wizi wa madawa wafichuliwa Uganda

Hebu fikiria, kuishi katika nchi ambako madaktari na maafisa wa madawa wanaiba dawa zinazookoa maisha, na zilizolengwa kupewa wagonjwa - ulafi wa wahudumu wa afya unaozidi wajibu wao wa kuwajali wagonjwa.

BBC Africa Eye imefanya upekuzi nchini Uganda kufichua jinsi wafanyakazi wa afya nchini humo walivyojitosa katika mitandao ya uhalifu.