Afcon 2019: Wachezaji maarufu waliotemwa Taifa Stars na Harambee Stars kombe la mataifa ya Afrika

Chanzo cha picha, Tff/ Twitter
Huku kombe la mataifa ya Afrika likitarajiwa kuanza kuumiza nyasi mnamo tarehe 22 mwezi huu nchini Misri , mataifa yanayoshiriki yameanza kutoa orodha za wachezaji wao watakaobeba bendera za mataifa yao katika michuano hiyo.
Hatahivyo tayari minong'ono imeanza kuhusu wachezaji walioorodheshwa kushiriki katika kombe hilo ambalo ndio la hadhi ya juu barani Afrika.
Wengi hususan mashabiki wa timu za Afrika Mashariki wanadai kwamba wachezaji muhimu waliofaa kushirikishwa katika mechi hizo walitemwa kwa sababu moja ama nyengine huku wengine wakikosa sababu zozote za kutoshirikishwa.

Chanzo cha picha, Tff/Twitter
Walio nje Tanzania
Nchini Tanzania kwa mfano wakati benchi la kiufundi la timu ya Taifa stars lilipokuwa likitoa orodha ya mwisho ya wachezaji 23 watakaoshiriki katika fainali hizo za AFCON, kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya, beki Kiraka Abdi Banda na mshambuliaji Shaban Chilunda ni mioingoni mwa nyota tisa walioenguliwa kikosini.
Kulingana na gazeti la Mwananchi, licha ya kuteuliwa kwenye kikosi cha awali, watatu hao wanaocheza soka la kulipwa katika nchi za Hispania, Afrika Kusini na Misri wameshindwa kupenya kwenye kikosi cha wachezaji 23 ambao kisheria ndio wanaopaswa kushiriki fainali hizo.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Kocha Emmanuel Amunike ameshindwa kumjumuisha Banda anayechezea klabu ya Baroka FC ya Afrika Kusini na badala yake ameamua kuwajumuisha kundini Ally Mtoni 'Sonso' wa Lipuli na nyota wa
Mbao FC, Vincent Philipo kulingana na gazeti la Mwananchi.
Kwa upande mwengine Kichuya anayechezea klabu ya ENPPI ya Misri, ameshindwa kufua dafu mbele ya Farid Mussa, Thomas Ulimwengu na Yahya Zayd, gazeti hilo limeongezea.
Vilevile hakukuwa na nafasi kwa mshambuliaji Shabani Chilunda ambaye hivi karibuni alivunja mkataba na klabu ya CD
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Tenerife ya Hispania kwa kutopata nafasi ya kutosha ya kucheza, na badala yake kocha Emmanuel Amunike amemuita mshambuliaji aliyetimuliwa na klabu ya Botswana Defence Force XI, Rashid Mandawa.
Kwa upande mwengine benchi la ufundi la Taifa Stars lilimpatia nafasi mshambuliaji Adi Yussuf ambaye hivi karibuni alitia saini mkataba wa kujiunga na Blackpool inayoshiriki Ligi ya Daraja la pili Uingereza.
Hata hivyo, hakukuwa na nafasi kwa nyota wa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 'Serengeti Boys', Kelvin John kama ilivyo kwa kipa wa timu ya Taifa chini ya umri wa miaka 20, Claryo Boniface.
Walioenguliwa Harambee Stars
Nchini Kenya Kocha wa Harambee Stars Sebastien Migne alimuacha nje kiungo wa kati wa klabu ya Zesco Anthony Akumu kutoka orodha ya wachezaji 23 watakaoshiriki katika michuano hiyo ya Juni 22 mjini Cairo.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3
Beki wa Afrika Kusini Brian Mandela tayari alikuwa amewekwa nje baada ya kupata jeraha , ikimaanisha kwamba kocha Migne alikuwa na wachezaji wengine watatu zaidi wa kuwatema kutoka kikosi chake cha wachezaji 27 ambacho kilikuwa nchini Ufaransa kutoka tarehe 30 mwezi Mei.
Winga Christopher Mbamba atalazimika kusubiri ili kuiwakilisha Kenya kwa mara ya kwanza.
Mchezaji wa Ureno Winga Clifton Miheso alikuwa mwathiriwa mwengine katika kikosi cha mwisho cha Migne ijapokuwa ni kutemwa kwa Akumu ambako kumewashanagazaa mashabiki wengi.
Kiungo huyo wa kati amekuwa kiungo muhimu katika klabu yake ya Zambia ijapokuwa hajakuwa akishirikishwa mara kwa mara katika mechi nne za kufuzu katika kipute hicho tangu mkufunzi huyo wa Ufaransa alipochukua hatamu.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 4
Mchezaji Allan wanga ambaye amekuwa akiongoza katika ufungaji wa magoli katika ligi ya kenya pia ni miongoni mwa Waathiriwa wa shoka la kocha Migne .
Mbali na Wanga kipa wa kariobangi Sharks Brian Bwire ambaye licha ya kujumuishwa katika kikosi hicho hapo awali alizua mjadala mkubwa.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 5
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 6
Hatahivyo alitemwa katika kikosi hicho pamoja na kiungo wa kati wa AF leopard Whyvonne Isuza.
Mchezaji Musa Mohammed ambaye alipata jeraha katika mechi ya kufuzu kombe la Afcon dhidi ya Madagascar siku ya Ijumaa ameorodheshwa katika orodha hiyo pamoja na Abud Omar ambaye pia alipata jeraha dogo kabla ya mechi hiyo kukamilika.












