Afa kwenye Ndege kwa kumeza dawa za kulevya

Ramani ikinyesha mji wa Hermosillo katika jimbo la Sonora nchini Mexico
Muda wa kusoma: Dakika 1

Mwanaume mmoja raia wa Japan, amepoteza maisha ndani ya Ndege akitokea Mexico City baada ya kumeza kete 246 za Cocaine.

Ndege hiyo, iliyokuwa ikielekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Narita nchini Japan ililazimika kutua kwa dharura katika jimbo la Sonora nchini Mexico mwanaume huyo alipoanza kupoteza fahamu.

Mamlaka zimesema mtu huyo aliyejulikana kwa jini la Udo N, alipoteza maisha baada ya ubongo wake kujaa maji kutokana na matumizi ya madawa kupita kiasi.

Kwa mujibu wa taarifa ya mwanasheria mkuu wa jimbo la Sonora, Kete zilizokua na urefu wa sentimita 2.5 na upana wa sentimita 1 zilikutwa tumboni na kwenye utumbo wakati wa uchunguzi.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Abiria wengine 198 waliobaki waliendelea na safari baada ya kutua kwa dharura katika mji wa Hermosillo.

Mamlaka za Mexico zimesema zitaendelea na uchunguzi.