Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanga wanaohangaisha wanakijiji kwa mazingaombwe usiku kucha Kenya
Kwa vizazi vingi tu, wakaazi wa maeneo ya vijijini wamelalamika kuhusu wanga wanaowahangaisha usiku kucha. Inasemekana ni wanakijiji waliopagawa na mapepo yanayowashurutisha kuwahangaisha na kuwaongopesha majirani zao usiku.
Lakini hakuna anayafahamu ni akina nani na lengo lao ni lipi.
Kwa niaba ya BBC Africa Eye, mwandishi Tom Odula amechungunza mazingaombwe hayo, na kuangazia ukweli katika kinachoaminika kuhusu wanga hao na kutoa picha ambazo hazijawahi kuonekana za wanga wakiwa kazini.