Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watoto wanaougua 'microcephaly' pwani ya Kenya watelekezwa
Baadhi ya familia katika kaunti ya Kilifi nchini Kenya wamekuwa wakijifungua watoto wenye hali isio ya kawaida.
Hali hiyo inayojulikana kama microcephaly husababisha ubongo wa mtoto usikuwe kama unavyohitajika kawaida na hivyobasi kusababisha hali ya mtoto kuwa na kichwa kidogo ikilinganishwa na watoto wengine umri wao.
Jamii imekuwa ikiwatelekeza watoto wenye hali hiyo na wamekuwa wakiwachukuliwa kama laana na wanaosababisha majanga kama alivyogundua mpiga picha wetu Anthony Irungu.