Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Waihiga Mwaura kutoka Kenya ashinda tuzo la BBC la Komla Dumor
Mwandishi wa habari mkenya na mtangazaji wa televisheni ndiye mshindi wa mwaka huu wa tuzo la BBC la Komla Dumor.
Waihiga Mwaura ni msomaji wa habari wa jioni kwenye kituo kinachotazamwa sana Kenya cha Citizen.
Kama sehemu ya tuzo hiyo, kwa miezi mitatu atakuwa kwenye ofisi ya BBC mjini London na baadaye kurudi Afrika kuendelea na kazi.