Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wavuvi watumia kondomu kulinda simu zao baharini pwani Kenya
Wavuvi kutoka pwani ya Kenya huko mjini Mombasa wamebuni mbinu mpya ya kulinda mawasiliano yao katika bahari ya Hindi. Wameanza kutumia mipira ya kondomu ili kulinda simu zao za mkononi , swala ambalo limewashangaza wengi. Hatua hiyo imerahisisha mawasiliano yao na wenzao walio nchi kavu iwapo kuna hatari yoyote mbali na wateja wao.