Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
BBC Africa Eye: Kituo cha kurekebisha tabia ambapo wagonjwa huteswa Kenya
Uchunguzi wa BBC Africa Eye umefichua kuwa wanawake na wanaume wa kisomali wamekuwa wakifanyiwa mateso na kunyanyaswa katika vituo vya kurekebisha tabia Afrika Mashariki. Vituo hivyo vinadaiwa kuwa vinawarekebisha wale wanaokwenda kinyume na utamaduni wa kisomali na dini, vikiwashutumu kutumia mihadarati na kuwa na tabia zisizo za kiislam. Lakini kama alivyobaini Jamal Osman wanafanyiwa mateso makali.