Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kitanzini: Eneo lililopata jina kutokana na kitanzi cha Mjerumani
Maeneo mengi Afrika Mashariki unapotaja majina ya mahala fulani, mara nyingi huendana na sifa za eneo hilo.
Huko mkoani Iringa nyanda za juu Kusini mwa Tanzania, kuna eneo lijulikanalo kama kitanzini, likiwa maarufu kwa wizi na ukabaji.
Eneo hilo lilikua ni sehemu ya kujinyongea watu kipindi cha ukoloni, hivyo wengi huamini damu ya watu walionyongwa ni matokeo ya matendo yanayoendelea hivi sasa.
Mwandishi wetu Eagan Salla alitembelea eneo hilo na kuzungumza na watu ambao wana kumbukumbu za kitanzi hicho.