Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtalii Mmarekani aliyegeuka na kuwa mwenyeji Lamu, Kenya
Mji wa Amu unaopatikana kaunti ya Lamu katika pwani ya Kenya huvutia watalii wengi kwa utulivu wake na watu wanaopenda wageni.
Baadhi ya watalii hufika na baadaye wakaamua kuishi hapo.
Mmoja wao ni Hadija Ernest kutoka Marekani ambaye ameolewa na mwenyeji wa Amu.
Mwandishi wa BBC John Nene alikutana na Hadija pamoja na mumewe Bwanaadi Issa Ali ambaye ni mvuvi na amezungumza nao kuhusu maisha yao.