Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uhaba wa nyanya Afrika Mashariki unasababishwa na nini?
Wakazi wa Afrika mashariki wamekuwa wakizungumzia kuadimika kwa nyanya siku za hivi karibuni. Katika baadhi ya masoko,nyanya inauzwa bei ya juu kuliko hata tufaha, tunda ambalo kwa kawaida huwa ndilo ghali mno maeneo mengi Afrika. Uhaba huu wa nyanya unadaiwa kusababishwa na mvua kubwa ambayo ilinyesha maeneo mengi mwishoni mwa mwaka jana.