Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanamuziki Joseph Shabalala afariki dunia
Joseph Shabalala, ambaye alisaidia kutanguliza sauti ya muziki wa jadi wa Kizulu ulimwenguni, amefariki akiwa na umri wa miaka 78. Mwanamuziki huyo alijulikana sana kama mwanzilishi na mkurugenzi wa kikundi cha wanamuziki cha Ladysmith Black Mambazo,ambacho kilishinda tuzo tano za Grammy na kuhusishwa sana kwenye albumu ya Paul Simon ya Graceland.