Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 12.07.2024

.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Aliyekuwa kocha wa Liverpool Jurgen Klopp

Marekani wamemfanya meneja wa zamani wa Liverpool Jurgen Klopp kuwa mgombea wao mkuu kuchukua nafasi ya Gregg Berhalter kama kocha wa taifa hilo. (Independent)

Klopp havutiwi na mpango wa Marekani na angependa kupumzika kuwa kocha . (Athletic – Subcsription Required )

Klopp pia anatakiwa na nchi yake ya Ujerumani. (TeamTalks)

Al-Ittihad wanakaribia kumnasa winga wa Aston Villa Mfaransa Moussa Diaby, 25. (Yahoo)

Al-Ittihad wako kwenye mazungumzo na kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Casemiro, 32. (L'Equipe – In French)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Casemiro

Beki wa Bayern Munich Mholanzi Matthijs de Ligt, 24, anataka kujiunga na Manchester United mara moja. (Sky Sports)

Bayern wanataka euro 50m (£38.7m) kwa De Ligt. (90min)

Crystal Palace wameazimia kutomuuza winga wa Uingereza Eberechi Eze, 26, kwa Tottenham au Manchester United. (Football Insider)

Nice wanavutiwa na beki wa Luton Town mwenye umri wa miaka 22 Teden Mengi. (Foot Mercato – In French)

Arsenal wamewasilisha ombi la kwanza kwa mlinda lango wa Ajax Tommy Setford mwenye umri wa miaka 18. (Fabrizio Romano).

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Joao Neves

Benfica wamekataa ofa kutoka kwa Paris St-Germain na Manchester United kwa ajili ya kiungo wa kati wa Ureno Joao Neves, 19. (A Bola – In Portugal)

AC Milan wanavutiwa na beki wa RB Salzburg Mserbia Strahinja Pavlovic, 23, ambaye pia anasakwa na Newcastle. (Calciomercato – IN Italy)

West Ham wamezuia nia ya Manchester City na watamweka kiungo wa kati wa Uingereza Chinaza Nwosu mwenye umri wa miaka 16 kwenye akademi yao. (Football Insider)

Chelsea wamemaliza harakati zao za kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Mhispania Samu Omorodion, 20. (Marca Spanish)

Imetafsiriwa na kuchapishwa na Seif Abdalla