Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Baba Samatta: Uingereza ndio kila kitu kwenye kandanda
Baba wa nahodha wa Tanzania Mbwana Samata anajivunia mafanikio ya mtoto wake katika ulimwengu wa kandanda.
Mzee Ally Pazi Samatta ameielza BBC kuwa imekuwa ni ndoto yao yeye na Mbwana siku moja kuona mshambuliaji huyo akitua Uingereza na kusakata kambumbu.
Ndoto hiyo inakaribia kukamilika wakati huu ambapo Aston Villa inatumai kukamilisha makubaliano ya dau la £10m kumsajili mshambuliaji huyo wa klabu ya Genk ya Ubelgiji.