Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtanzania Alice Ahadi Magaka alivyopata wazo lililomshindia Tuzo ya Malkia
Tuzo ya Malkia wa Uingereza kwa viongozi vijana hutolewa kila mwaka kama njia moja ya kuitambua kazi inayofanywa na vijana katika jamii mbalimbali za mataifa ya Jumuiya ya Madola.
Vijana waliofanikiwa huletwa Uingereza ili kukutana na wafanyabiashara mbalimbali na pia kupata nafasi zaidi ya kubadilishana mawazo.
Kati ya walioalikwa mwaka huu ni Alice Ahadi Magaka, kutoka Tanzania, ambaye alitutembelea katika studio zetu hapa London. Anaanza kwa kuelezea mradi wake unahusu nini.