Fred anayetarajiwa kujiunga na Man United apata jeraha katika mazoezi

Chanzo cha picha, PA
Kiungo wa kati wa Brazil Fred, anayetarajiwa kujiunga na klabu ya Manchester United amepata jeraha katika kifundo chake cha mguu katika mazoezi kabla ya kuanza kwa kombe la dunia.
United wamekubaliana dau la £47m kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kutoka klabu ya Shakhtar Donetsk huku uhamisho huo ukitarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Chanzo cha picha, EPA
Daktari wa timu ya Brazil Rodrigo Lasmar alilitaja jeraha hilo lililotokea mjini London kuwa lenye maumivu makali katika mguu wake.
Brazil inaanza kampeni yake ya kombe la dunia dhidi ya Switzerland tarehe 17 mwezi Juni.

Chanzo cha picha, Reuters
Washindi hao mara tano wa kombe la dunia baadaye watacheza katika kundi E dhidi ya Costa Rica na Serbia nchini Urusi.
Lasmar aliongezea: kwa sasa ni mapema mno kusema chochote kuhusu hali yake. Siku ya Ijumaa tutaangalia tujue kitakachofanyikana kuamua iwapo tunahitaji kufanya uchunguzi wowote ama la.









