Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Shangwe Uganda kufurahia kufuzu AFCON 2017
Sherehe zimekuwa zikiendelea kote nchini Uganda kufuatia timu ya taifa ya nchi hiyo kufuzu kucheza fainali za kombe la mataifa ya Afrika baada ya kusubiri kwa kipindi cha karibu miaka 40.
Mara ya mwisho Uganda ilicheza Kombe la mataifa ya Afrika mwaka 1978.
Wamefuzu tena baada ya kuishinda Comoro 1-0 mjini Kampala. Omar Mutasa alikuwepo na ana maelezo zaidi.