Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Niger yasimamishwa uanachama na Umoja wa Afrika baada ya mapinduzi

Umoja wa Afrika (AU) umeisimamisha Niger kutoka kwa shughuli zake zote baada ya mapinduzi ya kijeshi mwezi uliopita.

Moja kwa moja

  1. Ujumbe wa Kenya wakutana na polisi wa Haiti kutathmini usalama

    Ujumbe wa Kenya umefanya mikutano na maafisa wa polisi wa Haiti, wiki kadhaa baada ya serikali ya Kenya kujitolea kuongoza timu ya kimataifa katika kukabiliana na ghasia kali za magenge nchini humo.

    Haiti imekumbwa na ghasia mbaya tangu kuuawa kwa Rais wa nchi hiyo Jovenel Moïse miaka miwili iliyopita.

    Ghasia hizo zimeongezeka tangu Waziri Mkuu wa Haiti Ariel Henry alipoomba msaada kwa mara ya kwanza Oktoba mwaka jana, na kusababisha Marekani kuwahamisha wafanyakazi wake wa kidiplomasia.

    Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulisema kuwa zaidi ya watu 2,439 waliuawa, 902 walijeruhiwa na 951 kutekwa nyara katika nusu ya kwanza ya Januari.

    Ujumbe wa Kenya uliwasili katika mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince, Jumapili na unatarajiwa kuondoka Jumatano, baada ya majadiliano zaidi na waziri mkuu.

    Umepewa jukumu la kutathmini hali nchini, ambayo itaarifu juhudi za kuingilia kati zinazoungwa mkono na UN na Marekani. Kenya pia inatarajiwa kuongoza juhudi za kukabiliana na hali hiyo kwa kutuma maafisa 1,000 wa polisi nchini Haiti.

    Nchi za Caribbean kama Jamaica, Bahamas, Antigua na Barbuda na Trinidad na Tobago pia zimeahidi kutuma vikosi vyake kusaidia polisi wa Haiti.

  2. Waziri wa zamani wa mafuta wa Nigeria ashtakiwa kwa kupokea hongo

    Polisi wa Uingereza wanasema wamemshtaki waziri wa zamani wa mafuta wa Nigeria, Diezani Alison-Madueke, kwa makosa ya kupokea hongo.

    Shirika la Kitaifa la Uhalifu la Uingereza lilisema lilishuku kuwa alipokea hongo kama malipo kwa kutoa kandarasi za mamilioni ya dola za mafuta na gesi.

    Bi Alison-Madueke, ambaye pia ni rais wa zamani wa OPEC, alihudumu katika utawala wa kiongozi wa zamani wa Nigeria Goodluck Jonathan kuanzia 2010 hadi 2015.

    Anashukiwa kufaidika na makumi ya maelfu ya dola taslimu, safari za ndege kwa jeti za kibinafsi, likizo za kifahari kwa familia yake na matumizi ya mali nyingi za London.

    Anakanusha mashtaka. Polisi wanasema kwa sasa anaishi London na atafikishwa mahakamani mwezi Oktoba.

  3. Mwanamke mmoja atuhumiwa kuiba majeneza Kenya

    Mfanyakazi wa mauzo katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, ameshtakiwa kwa wizi wa majeneza mawili na vishikizo 26, kulingana na ripoti za ndani.

    Maureen Khikani, ambaye alikuwa mfanyakazi wa Huduma ya Mazishi ya Mtakatifu Augustine, anadaiwa kuiba vitu hivyo kwa muda wa wiki moja mwezi Mei mwaka jana.

    Anakanusha mashtaka yote. Majeneza hayo yalikuwa na thamani ya shilingi 90,000 za Kenya ($622, £488) na mipini ilikuwa $810. Hakimu wa mahakama ya Milimani Ben Mark Ekhubi amemuachilia kwa dhamana ya $1,380.

    Wakili anayemwakilisha Bi Khikani alikuwa ametoa wito wa kuachiliwa kwa masharti nafuu zaidi, akisisitiza jukumu lake kama mama asiye na mwenzi.

  4. Watoto wawili waokolewa kutoka kwa kundi lililokwama kwenye gari la kebo la Pakistan

    Waokoaji wamefaulu kumvuta mtoto wa pili kutoka kwa gari la kebo, kulingana na msemaji wa shirika la uokoaji na afisa wa wilaya.

    Shirika la habari la Reuters linaripoti kuwa wanafunzi watano na mwalimu mmoja bado wako ndani wakisubiri kuokolewa. Jeshi la Pakistan lilifanya uokoaji mara mbili za kwanza katika operesheni hatari iliyotatizwa na upepo mkali.

    Afisa wa polisi, Muhammad Amjad, amethibitisha kuokolewa kwa watoto wawili.

    Madaktari wapo kwenye helikopta walikotua, na wanafanya uchunguzi wa kimatibabu. Afisa wa polisi anasema watoto wote wako sawa.

    Kulingana na picha mtandaoni, gari hilo la kebo limekwama katikati ya bonde lenye kina kirefu katika mkoa wa Khyber Pakhtunkhwa.

    Uokoaji unaonekana kuwa mgumu kutokana na upepo mkali na wasiwasi kwamba rota za helikopta zinaweza kuharibu zoezi afisa wa uokoaji katika eneo hilo aliiambia Reuters.

  5. Pep Guardiola: Kocha wa Manchester City kukosa mechi mbili zijazo baada ya upasuaji mdogo wa mgongo

    Kocha wa Manchester City Pep Guardiola anatazamiwa kukosa mechi mbili zijazo za timu yake baada ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo.

    Guardiola, 52, alikuwa akisumbuliwa na kile City walisema kuwa ni "maumivu makali" ya mgongo na alisafiri hadi Barcelona kwa ajili ya "operesheni ya dharura" lakini "ndogo".

    City itacheza na Sheffield United siku ya Jumapili na kuwakaribisha Fulham tarehe 2 Septemba katika Uwanja wa Etihad.

    Guardiola anatarajiwa kurejea kazini baada ya mapumziko.

    Meneja Msaidizi Juanma Lillo atachukua nafasi ya mazoezi ya kikosi cha kwanza.

    City ilisema operesheni hiyo, iliyofanywa na Dkt Mireia Illueca, ilikuwa ya "mafanikio" na kuwa "atapona na kurejea Barcelona".

    Taarifa hiyo iliongeza: "Kila mtu katika Manchester City anamtakia Pep ahueni ya haraka, na anatazamia kumuona akirejea Manchester hivi karibuni."

    Guardiola aliiongoza klabu hiyo kutwaa Ligi Kuu, Kombe la FA na taji lao la kwanza la Ligi ya Mabingwa msimu uliopita. City wanashika nafasi ya pili kwenye Ligi ya Premia katika hatua za mwanzo, wakiwa sawa kwa pointi sita na vinara Brighton na Arsenal katika nafasi ya tatu, baada ya kuwalaza Burnley na Newcastle katika michezo yao miwili ya ufunguzi.

  6. Niger yasimamishwa na Umoja wa Afrika baada ya mapinduzi

    Umoja wa Afrika (AU) umeisimamisha Niger kutoka kwa shughuli zake zote baada ya mapinduzi ya kijeshi mwezi uliopita.

    Baraza la Amani na Usalama la AU lilitoa wito kwa nchi zote wanachama wake na jumuiya ya kimataifa kujiepusha na hatua zozote zinazoweza kuhalalisha utawala wa kijeshi nchini Niger.

    Ulikariri wito kwa viongozi wa mapinduzi kumwachilia huru Rais mteule Mohamed Bazoum.

    Umoja wa ukanda wa Afrika Magharibi, Ecowas tayari imetishia hatua za kijeshi kumrejesha kazini.

    Serikali ya Niger imesema kuwa utawala wa kiraia hauwezi kurejeshwa mpaka baada ya miaka mitatu, lakini hili limepuuzwa na Ecowas kuwa halikubaliki.

  7. Afrika Kusini yahodhi mkutano wa Brics, Jumuiya yatarajia ongezeko la wanachama

    Rais wa China Xi Jinping yuko nchini Afrika Kusini kwa ziara yake ya kwanza barani Afrika baada ya miaka mitano, ambayo sehemu yake atatumia kuhudhuria mkutano wa kilele wa Brics wa nchi zinazoinukia kiuchumi.

    Bw Xi, ambaye pia anafanya ziara ya kiserikali, aliwasili Johannesburg Jumatatu usiku na kukaribishwa na Rais Cyril Ramaphosa.

    Wawili hao wanakutana kabla ya mkutano mkuu, na wanatarajiwa kutia saini makubaliano ya nchi mbili kuhusu biashara na nishati.

    Pia siku ya Jumanne, Bw Xi atakuwa mwenyekiti mwenza wa Mazungumzo ya Viongozi wa China na Afrika na Bw Ramaphosa kando ya mkutano huo.

    Kuna ongezeko la nia ya uanachama wa Brics, huku zaidi ya nchi 20 - ikiwa ni pamoja na Algeria, Misri, Ethiopia, Iran na Argentina - zinazoomba kujiunga na kundi hilo, ambalo linaweza kuibuka kama mpinzani anayeonekana kutawala Magharibi katika masuala ya ulimwengu.

    Mkutano wa kilele wa mwaka huu utaangalia kukubaliwa kwa wanachama wapya.

    Jumla ya nchi 69 zimealikwa kwenye mkutano mkubwa wa Brics nchini Afrika Kusini, zikiwemo mataifa yote ya Afrika.

  8. Zoezi la kuwaokoa watu wanane walionasa kwenye gari la kebo linaendelea Pakistan

    Uokoaji unaendelea kwa watu wanane, wakiwemo watoto sita, waliokwama kwenye gari la kutumia nyaya (Cable car) kwenye bonde kaskazini-magharibi mwa Pakistan.

    Kundi hilo lilikuwa likielekea shuleni wakati moja ya nyaya hizo ilipokatika, na kuiacha ikining'inia mita 274 (futi 900) juu ya ardhi, maafisa walisema.

    Kaimu Waziri Mkuu wa Pakistan amewaamuru waokoaji kufika kwenye tukio la "kuogofya" huko Battagram.

    Helikopta za jeshi zimefika kwenye gari lakini hali ya uokoaji haijulikani. Abiria hao wanane walinaswa kwa takribani saa nne kabla ya helikopta ya kwanza kufika, chombo cha habari cha Dawn.com kiliripoti.

    Tukio hilo lilitokea yapata saa 07:00 kwa saa za huko (02:00 GMT) siku ya Jumanne katika eneo la mbali, la milimani ambapo magari ya nyaya ni viunganishi vya kawaida kwa wakazi.

    "Mungu tusaidie," Gulfraz, mwanaume aliyekwama kwenye gari hilo, alikiambia kituo cha televisheni cha Pakistani cha Geo News kwa njia ya simu.

    Alithibitisha watu wanane walikuwa ndani ya chombo hicho. Mmoja wa wanafunzi hao alikuwa amepoteza fahamu katika muda wa saa tatu zilizopita, alisema na kuongeza kuwa wanafunzi walikuwa na umri wa kati ya miaka 10 na 15.

    "Watu katika eneo letu wamesimama hapa na kulia," Gulfaraz alisema, akizitaka mamlaka kutuma msaada wa haraka.

    Kulingana na picha mtandaoni, gari hilo la kebo limekwama katikati ya bonde lenye kina kirefu katika mkoa wa Khyber Pakhtunkhwa.

    Uokoaji unaonekana kuwa mgumu kutokana na upepo mkali na wasiwasi kwamba rota za helikopta zinaweza kuharibu zoezi afisa wa uokoaji katika eneo hilo aliiambia Reuters.

    Helikopta moja tayari imerejea kutoka kwa safari ya uchunguzi huku nyingine ikitumwa hivi karibuni, aliongeza. Mwalimu wa eneo hilo aliiambia Dawn.com kwamba takriban watu 150 husafiri kwa gari la kebo kwenda shule kila siku kwa sababu ya ukosefu wa njia za usafiri katika eneo hilo.

  9. Afrika ya Kati yaidhinisha mihula ya urais isiyo na kikomo madarakani,

    Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati imeidhinisha matokeo ya kura ya maoni ya mwezi Julai ambayo yanaongeza urefu wa muhula wa urais hadi miaka saba, lakini inamruhusu rais kugombea wadhifa huo mara nyingi apendavyo.

    Mahakama ilitangaza kwamba idadi kubwa ya 95% iliidhinisha kura, na waliojitokeza kuwa zaidi ya 57%.

    Sheria mpya inaunda ofisi ya makamu wa rais, aliyeteuliwa na rais, na bunge la umoja, na kuondoa seneti. Pia inapiga marufuku wanasiasa wenye uraia pacha kuwania urais na kuongeza idadi ya majaji wa mahakama ya juu kutoka tisa hadi 11.

    Mahakama ya juu ilikuwa Septemba mwaka jana ilitupilia mbali kamati iliyopewa jukumu la kuandaa sheria mpya kabla ya rais wa mahakama hiyo, Daniele Darlan, kustaafu kwa lazima.

    Vyama vikuu vya upinzani nchini humo na mashirika ya kiraia yamehimiza kususia, vikisema sheria iliyorekebishwa iliundwa ili kumweka Rais Faustin-Archange Touadéra madarakani maisha yake yote.

    Walishutumu kamati ya marekebisho ya katiba kwa kuchukua maagizo kutoka Urusi. Rais Touadéra anaungwa mkono na mamluki wa Urusi Wagner.

    Wapiganaji wa ziada walikuwa wamefika kabla ya kura ya maoni ili kulinda usalama. Nchi hiyo yenye utajiri wa almasi na dhahabu ambayo haina bahari imekumbwa na migogoro na misukosuko ya kisiasa kwa sehemu kubwa ya historia yake tangu ilipojinyakulia uhuru kutoka kwa Ufaransa mwaka 1960.

  10. Watoto adimu wa chui milia wanaonekana kwa mara ya kwanza Ujerumani

    Watoto wawili wa chui milia, ambao ni spishi ndogo na adimu walio katika hatari ya kutoweka, wameonyeshwa hadharani kwa mara ya kwanza tangu kuzaliwa kwao mnamo Juni. Chui milia wa Sumatra hupatikana katika kisiwa cha Indonesia cha Sumatra pekee.

  11. Familia ya mwanariadha wa Rwanda aliyeuawa Kenya yatoa wito wa "ukweli na haki"

    Familia ya mwanariadha wa Rwanda aliyeuawa katika mji maarufu wa magharibi mwa Kenya inatoa wito wa "ukweli na haki" kwa mtoto wao ambaye "alikuwa akifuatilia shauku yake ya kukimbia na kuwa bora kichezo".

    Polisi inasema inachunguza tukio hilo lililosababisha kifo cha Siragi Rubayitaambacho vyombo vya habari vya eneo hilo vilikihusishwa na suala la "mzozo wa mapenzi " katiya Bw Rubayita, na wanariadha wawili wa Kenya wa kike na kiume ambao kwa sasa ni washukiwa wakuu wa kifo hicho.

    Bw Rubayita, 34, mwanariadha wa masafa marefu ambaye alikuwa akifanya mazoezi katika eneo la Iten, Kaunti ya Elgeyo Marakwet,kabla ya mashindano nchini Italia, aliuawa katika "kitendo kisicho na maana cha vurugu... wakati mwanariadha mwenzake na mpenzi wake walipomwalika nyumbani kwao usiku kabla ya kuondoka kwake," familia yake ilisema katika taarifa.

    Nasra Bishumba,dada wa Bw Rubayita, aliiambia BBC kwamba kaka yake alitarajiwa kurudi nyumbani Kigali siku yaIjumaa kabla ya kuondoka kwenda Italia.

    Alisema wakufunzi wakee huko Iten walikuwa "wamejitosa katika kumtafuta wakati mwanariadha waliyelala naye chumba kimoja alipotoa tahadhari kuwa hajarejea kulala.

    "Baada ya kutuarifu, mara moja walianza kufanya kazi na polisi na hivyo ndivyo watuhumiwa walivyokamatwa."

    Baadhi ya vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kuwa mwanariadha wa kiume wa Kenya hakufurahishwa na uhusiano kati ya mwanariadha huyo wa Rwanda na mwanariadha wa kike wa Kenya.

    Uchunguzi wa mwili wa Bw Rubayita unatarajiwa kufanyika , nafamilia yake imetuma ujumbe wake Iten"kumrudisha nyumbani ambako tunatarajia kumpa upendo na kumuenzi kulingana na alivyokuwa mtoto na kaka wa kipekee ", dada yake ameiambia BBC.

    Ubalozi wa Rwanda nchini Kenya umeiambia BBC katika taarifa yake kwamba "mwanadiplomasia kutoka ubalozi huo yuko tayari kufuatilia kesi hiyo".

    Rubayita ameiwakilisha Rwanda katika mashindano ya kimataifa barani Afrika na Ulaya, mwezi Juni alikimbia mbio za nusu marathon kwa muda wa saa 1:05:34 katika mbio za mji wa Kigali -Kigali International Peace Marathon akichukua nafasi ya 13.

  12. Mason Greenwood: Gary Neville akosoa jinsi Manchester United inavyoshughulikia uchunguzi

    Gary Neville anasema jinsi Manchester United inavyoshughulikia uchunguzi wa Mason Greenwood imekuwa hatua ya "ya kutisha sana" na haina uongozi thabiti.

    Greenwood, 21, ataondoka katika klabu hiyo kwa makubaliano ya pande zote mbili baada ya uchunguzi wa ndani wa miezi sita.

    Ilikuja baada ya mashtaka dhidi ya mchezaji huyo, ikiwa ni pamoja na kujaribu kubaka na kushambulia,kuondolewa mwezi Februari.

    "Ilikuwa wazi tangu siku ya kwanza kwamba hataichezea Manchester United tena," alisema beki wa zamani Neville.

    Akizungumza kwenye Sky Sports Monday Night Football, Neville, 48, ambaye alichezea mechi 602 , aliongeza: "Mchakato wa kufika huko umekuwa mbaya sana. Unapokuwa na hali muhimu, na hali ngumu kama hii, inahitaji uongozi thabiti wenye mamlaka. Na hiyo inatoka juu sana. Manchester United hawana hilo."

    Mchambuzi mwenzake na kiungo wa kati wa zamani wa England Karen Carney alisema suala hilo "lilishughulikiwa vibaya" na ilikuwa "hali isiyofurahisha sana kwangu".

    Mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Greenwood alikamatwa Januari 2022 kufuatia madai kuhusu nyenzo ambayo ilichapishwa mtandaoni.

    Unaweza pia kusoma

  13. Bukavu: Kifo cha msichana aliyeuawa chawasikitisha raia wa DRC

    Baadhi ya wakazi wa mji wa Bukavu katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanasema wamesikitishwa na kushtushwa na binti huyo aliyeuawa na kuchomwa moto baada ya kupigwa na kundi la watu.

    Ilitokea siku ya Jumamosi baada ya watu kusema kuwa msichana huyo alinaswa akiwa na mtungi( gerikani) lililojaa petroli karibu na mahali palipochomwa moto, wakimtuhumu kuwa ndiye anayeendesha mashambulizi ambayo yamekuwa yakiendelea kwa siku nyingi katika eneo la Panzi, Bukavu.

    Mmoja wa waandishi wa habari wa kujitegemea wanaofanya kazi huko Bukavu aliambia BBC kwamba watu wengi walirusha vijiti, mawe na vitu vingine vya kuumiza na kumpiga msichana huyo mwenye umri wa miaka 17 hadi akapoteza fahamu.

    Justin Kabangu, mmoja wa wakazi wa Bukavu, aliambia BBC kwamba alifika eneo la tukio baada ya tukio hilo, na kusikia baadhi ya watu wakijutia kifo cha msichana aliyeuawa bila ushahidi wowote wa kile alichotuhumiwa.

    Alisema, “Inasikitisha kwamba watu wanamchukua mtoto kwa namna hiyo na kumlaumu na kumhukumu hivyo. Ni aibu na aibu kwetu.”

    BBC ilijaribu kuzungumza na mamlaka ya jimbo la Kivu Kusini kuhusu mauaji ya msichana huyu lakini haijawezekana kufikia sasa.

  14. Thaksin Shinawatra: Waziri Mkuu wa zamani mwenye uzushi arejea Thailand baada ya miaka 15

    Waziri mkuu wa zamani Thaksin Shinawatra amerejea Thailand baada ya miaka 15 uhamishoni, saa chache kabla ya kura itakayoamua ni nani atakuwa kiongozi wa nchi hiyo.

    Kiongozi huyo aliyefanikiwa zaidi aliyechaguliwa nchini Thailand kwa muda mrefu amekuwa akiogopwa na wanamfalme wahafidhina, ambao wameunga mkono mapinduzi ya kijeshi na kesi zenye utata mahakamani ili kumdhoofisha.

    Lakini sasa tajiri huyo shupavu na mwenye malengo ya kisiasa amerejea, huenda baada ya kufanya makubaliano ya kimya kimya na wale wale waliokiondoa chama chake katika mapinduzi ya mwaka 2014 ili kumzuia kutoka gerezani.Ana hukumu ya hadi miaka 10 kutoka kwa kesi za jinai ambazo anasema zilichochewa kisiasa.

    Alitua katika mji mkuu Bangkok saa 09:00 kwa saa za huko kwa ndege ya kibinafsi kutoka Dubai kupitia Singapore.Kulikuwa na shangwe, hotuba na nyimbo kutoka kwa mamia ya wafuasi wake waliochangamka huku Bw Thaksin hatimaye akitimiza ahadi nyingi alizoahidi kurejea.Wengi walikuwa wamesafiri usiku kucha kutoka ngome ya chama chake kaskazini-mashariki mwa Thailand kushuhudia tukio hilo.

    Lakini Bw Thaksin hakuweza kuwasalimia.Akiwa amezungukwa na binti zake wawili na mwanawe wa kiume, alitoka kwa muda mfupi kutoka kwenye uwanja wa ndege na kutoa heshima zake kwa picha ya mfalme na malkia.

    Unaweza pia kusoma

  15. Trump anasema atakamatwa siku ya Alhamisi katika kesi ya uchaguzi ya Georgia

    Donald Trump amesema anapanga kujisalimisha siku ya Alhamisi katika mahakama ya jimbo la Georgia kujibu mashtaka ya kubadilisha matokeo ya uchaguzi.

    Jaji mmoja mjini Atlanta ambaye anasimamia kesi ya rais huyo wa zamani ameweka dhamana ya $200,000 (£157,000).

    Makubaliano hayo yanasema Bw Trump anaweza kubaki huru akisubiri kesi yake ilimradi asijaribu kutishia au kuwatisha mashahidi.

    Bw Trump anakanusha mashtaka 13, yakiwemo ya ulaghai na taarifa za uongo.

    "Mshtakiwa hatafanya kitendo chochote cha kumtisha mtu yeyote anayejulikana kuwa mshtakiwa mwenza au shahidi katika kesi hii au kuzuia utendakazi wa haki vinginevyo," ilisema jalada la mahakama lililotumwa Jumatatu.

    "Hayo hapo juu yatajumuisha, lakini sio tu, machapisho kwenye mitandao ya kijamii au machapisho yaliyotolewa na mtu mwingine kwenye mitandao ya kijamii," agizo hilo linaongeza.

    Ilitiwa saini na Wakili wa Wilaya ya Fulton, Fani Willis, anayesimamia kesi hiyo, na mawakili wa Bw Trump.

    Baadaye siku ya Jumatatu Bw Trump alichapisha kwenye mtandao wake wa kijamii, Truth Social: "Je, unaweza kuamini? Nitaenda Atlanta, Georgia, Alhamisi KUKAMATWA na Wakili wa Wilaya ya Radical Left, Fani Willis."

    Unaweza pia kusoma

  16. Mkuu wa Wagner Prigozhin aonekana kwenye hotuba ya kwanza ya video tangu jaribio la mapinduzi

    Kiongozi wa Wagner Yevgeny Prigozhin ameonekana katika hotuba yake ya kwanza ya video tangu maasi yake kushindwa nchini Urusi, ambayo yanaashiria yuko Afrika.

    BBC haijaweza kuthibitisha ni wapi video hiyo ilirekodiwa.

    Video hiyo iliyotumwa kwenye chaneli za Telegram zinazohusishwa na kundi la mamluki la Wagner inaonyesha Prigozhin akiwa amevalia sare za kivita, akisema kundi hilo linaifanya Afrika "huru zaidi".

    Wagner inaaminika kuwa na maelfu ya wapiganaji katika bara hilo, ambapo ina shughuli kibiashara zenye faida kubwa.

    Wanajeshi wa Prigozhin wamejikita katika nchi zikiwemo Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) - ambapo mashirika ya kutetea haki za binadamu na Umoja wa Mataifa yanawatuhumu kufanya uhalifu wa kivita.

    Uingereza mwezi uliopita iliweka vikwazo kwa wakuu wawili wa operesheni za Wagner nchini CAR, ikiwatuhumu kwa mateso na mauaji ya raia.

    Wapiganaji wa Wagner pia wameshutumiwa na Marekani kwa kujitajirisha kwa mikataba haramu ya dhahabu katika bara hilo.

    Katika video hiyo, Prigozhin anasema Wagner inachunguza madini pamoja na kupambana na wanamgambo wa Kiislamu na wahalifu wengine.

    "Tunafanya kazi. Halijoto ni +50 - kila kitu tunachopenda. Wagner PMC inafanya uchunguzi na utafutaji, inaifanya Urusi kuwa kubwa zaidi katika mabara yote, na Afrika kuwa huru zaidi," Prigozhin anaweza kusikika akisema.

    Unaweza pia kusoma

  17. Vita vya Ukraine:Ukraine yashambulia na kuharibu ndege hatari ya Urusi ya kurusha mabomu ya masafa marefu

    Ndege kubwa ya Urusi ya kurudha mabomu ya masafa marefu imeharibiwa katika shambulio la ndege zisizo na rubani za Ukraine, kulingana na ripoti.

    Picha zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kuchambuliwa na BBC Verify zinaonyesha ndege ya Tupolev Tu-22 ikiwaka moto kwenye uwanja wa ndege wa Soltsy-2, kusini mwa St Petersburg.

    Moscow ilisema kuwa droniisiyokuwa na rubani ilipigwa na moto wa silaha ndogo lakini iliweza "kuharibu" ndege hiyo. Ukraine haijatoa maoni.

    Baadaye, walinzi wa anga wa Urusi walidungua ndege mbili zisizo na rubani katika mkoa wa Moscow, Meya Sergei Sobyanin alisema.

    Maafisa wa ulinzi walisema ndege nyingine mbili zisizo na rubani zilinaswa kwenye eneo la Bryansk, kaskazini-mashariki mwa mpaka wa Ukraine.

    Safari za ndege zilisitishwa katika viwanja vya ndege vitatu vikubwa zaidi vya Moscow, kulingana na vyombo vya habari vya serikali - lakini viwanja vya ndege viwili vikuu vya kimataifa huko Sheremetyevo na Domodedovo vilifunguliwa tena.

    Ndege ya kivita ya Urusi ya Tu-22 iliyoharibiwa inaweza kusafiri kwa kasi mara mbili ya sauti na imekuwa ikitumiwa sana na Urusi kushambulia miji ya Ukraine.

    Hata hivyo, picha zilizochapishwa kwenye mtandao wa kijamii wa Telegram zilionyesha moto mkubwa ukiteketeza ndege yenye koni ya kipekee ya Tu-22. BBC Verify ilichanganua picha hizo na inaamini kuwa ni za kuaminika.

    Shambulio hilo sasa linatoa taswira mpya ya uwezo wa Ukraine kushamulia malengo ndani kabisa ya Urusi.

    Kyiv katika miezi ya hivi karibuni imezindua makumi ya ndege zisizo na rubani kushambulia Moscow, safari ya maili mia kadhaa. Soltsy-2 iko karibu maili 400 (650km) kutoka mpaka wa Ukraine.

    Unaweza pia kusoma

  18. Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya moja kwa moja leo Jumanne, tarehe 22 , Agosti 2023