Mnyarwanda anayeshukiwa kumtusi Rais Kagame apinga kesi yake kuendeshwa faraghani,
Kesi ya Myarwanda anayeshukiwa kumtusi Rais Kagame apinga kesi yake kuwa faraghani.
Kesi ya Bi Idamange Yvonne anayeshtakiwa kukana mauaji ya kimbari na kumtusi rais wa Rwanda Paul Kagame imeendelea leo.
Mshitakiwa amepinga jopo la majaji wanaoendesha kesi hiyo baada ya jopo hilo kuamuru kuwa kesi itasikilizwa kwa faragha.
Mwanamke huyo aliyejipatia umaarufu kupitia vipindi vyake vya kuikosoa serikali ya Rwanda anataka kesi yake kusikilizwa hadharani jambo linalopingwa na mwendeshamashitaka akisema huenda likasababisha athari mbaya na mkanganyiko miongoni mwa wananchi.
Idamange anakanusha mashitaka dhidi yake akisema yeye ni mwanaharakati anayetetea demokrasia nchini.
Yvonne Idamange amepandishwa kizimbani leo kwa kutumia teknolojia ya video akiwa katika Gereza la Mageragere na jopo la majaji likiwa mjini Nyanza ,
Amesema mshukiwa aliyemtusi rais hadharani kwa kutumia Channel yake ya Youtube na sio lazima mahakama impe fursa tena kuendelea na kauliza zake na matusi.
"Rais ni mtu maalum ambaye ametukanwa hadharani na sasa unataka korti iwe njia ya kupitishia matamshi hayo?’’ alihoji mwendesha mashtaka.
Idamange na mawakili wake wamesema kesi lazima iendeshwe hadharani kwa sababu hata mashtaka dhidi yake yaliwekwa hadharani aliposhitakiwa na kusema katu hawezi kuhudhuria vikao vya kesi itakayoendeshwa kwa faraghani.
Baada ya kusikiliza pande zote mbili, jopo la majaji limekata kauli kuwa kesi itaendeshwa faraghhani ili kuepuka kuwepo kwa mkanganyiko miongoni mwa wananchi kutokana na kauli za mshukiwa Bi Yvonne Indamange.
Mara tu baada ya kusikia uamuzi wa korti Yvonne Idamange amesema anaamini hatapewa haki na kutangaza kupinga jopo la majaji.
Jaji alisema kwamba kutokana na uamuzi wa mshukiwa kupinga jopo , korti itaamua tarehe itakapounda jopo jingine, terahe nyingine ya kesi na namna kesi hiyo itakavysikilizwa.
Idamange Yvonne mwenye umri wa miaka 42 anayedai kuwa mwanaharakati na mtetezi wa demokrasia alikamatwa Aprili, 2021 kufuatia matamshi na video alizokuwa akiweka kwenye mtandao wake wa Youtube dhidi ya serikali.