Mazishi ya kitaifa ya rais wa Chad Idriss Déby
Itno yatafanyika Ijumaa katika mji mkuu wa nchi hiyo N'Djamena kabla ya kuzikwa
katika mkoa wake.
Aliuawa Jumatatu
katika eneo la mapigano dhidi ya wapiganaji wa Front for Change and Concord in Chad (Fact), kikindi
cha wanajshi kilichoundwa na maafisa wa kijeshi mwaka 2016.
Viongozi wa mataifa ya
Mali na Guinea wamewasili, na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron pia anawasili kuelekea mjini N'Djamena licha ya onyo kutoka kwa waasi
kwamba kiongozi huyo wa kigeni hapaswi kuhudhuria kwa sababu za kiusalama.
Baada ya kutolewa kwa heshima za kijeshi na hotuba
mbali mbali, sala itafanyika katika msikiti wa Grand Mosque uliopo N'Djamena.
Baadaye , mwili wa Bw Déby's
utasafirishwa kwa ndege hadi Amdjarass,
kijiji kidogo kilichopo karibu na mji anakotoka wa Berdoba, uliopo zaidi ya kilomita 1000 (maili
621) kutoka mji mkuu, karibu na mpaka wa Sudan.
Rais Déby alikuwa mtu
muhimu katika mkakati wa usalama katika kanda ya Sahel.
Baraza la kijeshi
linaloongozwa na mwanae, Jeneral Mahamat Idriss lilichukua madara baada ya kifo
chake naanaungwa mkono kwa kiasi kidogo na jeshi lakini anauungwa mkono na
mtawala wa Ufaransa.
Generali Déby, 37, amesema jeshi litafanya uchaguzi wa
kidemokrasia katika kipindi cha miezi 18 ijayo, lakini viongozi wa upinzani wamelaani
hatua yake ya kuchukua mamlaka na kuitaja kama mapinduzi na jenerali wa kijeshi
amesema maafisa wengi wanapinga uongozi wake wa mpito.
Ni mpango ambao pia
waasi waliupinga huku pia wakionya kuwa watasitisha kipindi kidogo
kilichokuwepo cha usitishaji mpigano.
Mgawanyiko ndani ya
jeshi na upinzani vinamaanisha kuwepo kwa ukosefu mkubwa wa usalama huku kukiwa
piwa nma changamoto za kiuchumi wakati Chad inaingia katika kipindi cha mpito .