Meli ya kijeshi ya Marekani yawasili Sudan baada ya meli ya Urusi
Meli ya kivita ya Marekani imetia nanga katika mwambao wa Sudan Port Sudan siku moja baada ya meli ya Urusi kuwasili katika bandari hiyo hiyo iliyopo katika bahari nyekundu.
Wanadiplomasia wa Marekani wanasema ziara ya pili ya meli ya kikosi cha wanamaji cha Marekani inaonesha utashi wa kuimarisha ushirikiano mpya baina ya nchi mbili.
Marekani iliiondoa Khartoum katika orodha ya nchi zinazodhamini ugaidi kufuatia kupinduliwa kwa rais wa zamani wa nchi hiyo Omar al-Bashir mwaka 2019.
Urusi inajenga ngome ya jeshi la majini karibu na bandari ya Port Sudan, yenye ukubwa wa kutosha kuweza kupokea meli nne za kijeshi na wanajeshi 300.