Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Tunachojua kuhusu aliyefyatua risasi wakati wa mkutano wa Trump

FBI ilimtaja Thomas Matthew Crooks mwenye umri wa miaka 20 kuwa "mhusika" .Aliuawa kwa kupigwa risasi na wana usalama.

Muhtasari

  • Trump 'anaendelea vyema' na anawashukuru maafisa wa usalama
  • Wizara ya afya inayosimamiwa na Hamas imesema watu 90 waliuawa katika shambulizi la Israel lililomlenga mkuu wa kijeshi
  • Tunachojua kuhusu aliyefyatua risasi wakati wa mkutano wa Trump
  • Kitendawili cha miili iliyogunduliwa jalalani Nairobi Kenya kuteguliwa
  • Euro 2024: England kukutana na Hispania katika fainali

Moja kwa moja

Lizzy Masinga

  1. Euro 2024: England kukutana na Hispania katika fainali

    Hispania imekuwa timu iliyosisimua zaidi katika mashindano na walikutanishwa na timu nzito katika droo ya mashindano haya. Katika awamu ya makundi waliishinda Italia Albania na Croatia kuongoza katika kundi hilo.

    Hii iliwasukuma kukutana na Georgia katika awamu ya timu 16 ambapo waliifunga timu hiyo 4-1.

    Katika robo fainali waliikaribisha Ujerumani na Dani Olmo alifunga bao la kwanza kabla ya Florian Wirtz kulisawazisha kunako dakika 89. Mikel Merino alilisukuma tobwe la ushindi katika muda wa ziada na kuipatia timu hiyo fursa ya kuingia katika nusu fainali dhidi ya Ufaransa.

    Katika kinachotajwa kuwa mechi bora zaidi. Mchuano kati ya Uhispania na Ufaransa ulisisimua.

    Randal Kolo Muani aliifungia Ufaransa bao la utangulizi lakini mawili ya haraka kutoka Lamine Yamal na Olmo yaliipatia Uhispania ushindi.

    Sasa ni England tu ndio kizuizi kwa miamba hiyo ya Uhispania kunyakua ubingwa.

    Safari ya England kueleka fainali Haijakuwa safari rahisi kwa England kufika katika fainali. Walianza kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Serbia kufuatia mkwaju wake Jude Bellingham.

    Sare ya 1-1 dhidi ya Denmark alafu sare nyingine ya 0-0 dhidi ya Slovenia iliwafanya kuibuka kidedea katika kundi lao. Katika mechi ya timu 16 England ilikutana na Slovakia katika mechi ilioingia katika muda wa ziada.

    Hatimaye Harry Kane alifanikiwa kufunga bao la ushindi. England ilifuzu katika robo fainali ambako ilikutana na Uswizina kupata ushindi wa 5-3 kupitia mikwaju ya penalti.

    England ilikuwana kibarua kigumu katika nusu fainali ilipotuna na miamba ya soka Uholanzi.

    Ollie Watkins alifanikiwa kufunga bao la ushindi katika dakika ya mwisho ya mechi hiyo. Sasa inapokutana na Uhispania katika fainali, msema kweli ni nani?

    Unaweza kusoma;

  2. Kitendawili cha miili iliyogunduliwa jalalani Nairobi Kenya kuteguliwa

    Kaimu Mkuu wa Polisi, Douglas Kanja ametoa matokeo ya uchunguzi wa awali ambao unaonesha kuwa maiti zote nane zilizopatikana katika jalala la Kware jijini Nairobi zilikuwa za kike ambazo zilikatwa vipande vipande.

    ''Nimewahamisha maafisa kutoka Kituo cha Polisi cha Kware ili kuhakikisha uchunguzi wa haki na usawa'' alisema mkuu huyo

    Itachukua siku 21 kwa polisi na mashirika ya uchunguzi nchini Kenya kutegua kitendawili cha miili hiyo.

    Katika hotuba kwa vyombo vya habari Jumapili, Kaimu Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja na Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) Mohamed Amin walihakikishia umma kwamba uchunguzi kuhusu mauaji hayo unaendelea, na baadhi ya watu wanaohusika wametambuliwa.

    Tukio hilo limeweka shinikizo kwa Rais William Ruto, ambaye ameapa kwamba wale waliohusika na mauaji hayo wataadhibiwa.

    "Sisi ni nchi ya kidemokrasia inayoongozwa na utawala wa sheria. Wale waliohusika katika mauaji ya kutatanisha Nairobi na sehemu nyingine yoyote ya nchi watawajibishwa," alisema katika chapisho kwenye ukurasa wa X, zamani Twitter.

    Kisa hicho ni tukio la hivi karibuni la kuhuzunisha nchini Kenya.

    Mwaka jana nchi iliachwa na hofu baada ya mabaki ya mamia ya watu wanaohusishwa na ibada ya siku ya maangamizi kugunduliwa katika mji wa pwani wa Bahari ya Hindi wa Malindi. Paul Nthenge Mackenzie alifikishwa mahakamani mjini Mombasa mapema wiki hii kwa tuhuma za ugaidi na mauaji kutokana na vifo vya wafuasi wake zaidi ya 440.

    Anakanusha madai hayo. Anadaiwa kuwahimiza wanaume, wanawake na watoto kujinyima kula ili "kukutana na Yesu", katika moja ya vibaya zaidi duniani vinavyohusiana na ibada.

    Unaweza kusoma;

  3. Tunachojua kuhusu aliyefyatua risasi wakati wa mkutano wa Trump

    FBI ilimtaja Thomas Matthew Crooks mwenye umri wa miaka 20 kuwa "mhusika" Aliuawa kwa kupigwa risasi na wana usalama.

    Crooks alikuwa akitoka Bethel Park huko Pennsylvania, karibu saa moja kutoka mahali ambapo mkutano huo ulifanyika .

    Alikuwa mfuasi wa Republican aliyesajiliwa, kulingana na rekodi za wapiga kura wa serikali Lakini kulingana na Reuters, alipokuwa na umri wa miaka 17, alitoa mchango wa $ 15 kwa ActBlue, kamati ya kisiasa ambayo inachangisha pesa kwa wanasiasa wa mrengo wa kushoto na wa Kidemokrasia.

    Maafisa polisi walisema siku ya Jumamosi Crooks hakuwa na kitambulisho chochote kwenye eneo la tukio na ilibidi kutambuliwa kwa kutumia njia nyingine. Sababu haijatambuliwa, lakini mamlaka inachukulia tukio hilo kama "jaribio la mauaji"

  4. Wizara ya afya inayosimamiwa na Hamas imesema watu 90 waliuawa katika shambulizi la Israel lililomlenga mkuu wa kijeshi

    Wizara ya afya inayoendeshwa na kundi la Hamas huko Gaza imesema takribani Wapalestina 90 wameuawa katika shambulio la anga la Israel kwenye eneo lililoteuliwa la kibinadamu.

    Takribani watu 300 wamejeruhiwa, kwa mujibu wa taarifa ya wizara ya afya, katika shambulio ambalo Israel inasema lilimlenga kiongozi mkuu wa Hamas Mohammed Deif na naibu wake Rafa Salama.

    Katika mkutano na waandishi wa habari Jumamosi jioni, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema "hakuna uhakika" kwamba yeyote kati yao ameuawa.

    shambulio hilo lilipiga eneo la al-Mawasi karibu na Khan Younis, ambalo jeshi la Israel limetaja kuwa eneo la kibinadamu.

    Shahidi aliyeshuhudia katika al-Mawasi aliambia BBC kwamba eneo la shambulio lilionekana kama "tetemeko la ardhi" lilikuwa limepiga.

    Video kutoka eneo hilo zinaonesha mabaki ya moshi na majeruhi waliomwaga damu yakipakiwa kwenye machela.

    BBC Verify imechambua picha za matokeo ya shsmbulio hilo, na kuthibitisha kuwa ulifanyika katika eneo lililooneshwa kwenye tovuti ya Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) kama eneo la kibinadamu.

  5. Trump 'anaendelea vyema' na anawashukuru maafisa wa usalama

    Donald Trump "anaendelea vyema" na anawashukuru maafisa wa kutekeleza sheria, kulingana na taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya nje ya Kamati ya Kitaifa ya Republican (RNC).

    Inasema "anatarajia kuungana nanyi nyote huko Milwaukee tunapoendelea na kongamano letu la kumteua kuhudumu kama rais wa 47 wa Marekani. Akiwa mteule wa chama chetu... [ataendelea] kushiriki maono yake ya Make America Great Again," taarifa ya kampeni ya Trump na RNC imeeleza.

    Trump aliwashukuru maafisa wa kutekeleza sheria na Huduma ya Siri kwa "majibu yao ya haraka".

    "Kikubwa zaidi naomba nitoe salamu za rambirambi kwa familia ya mtu aliyekuwa kwenye mkutano wa hadhara aliyeuawa, na pia kwa familia ya mtu mwingine aliyejeruhiwa vibaya, ni jambo la ajabu kuwa kitendo cha aina hii kinaweza kutokea katika nchi yetu, " alisema.

    "Hakuna kinachojulikana kwa wakati huu kuhusu mpiga risasi ambaye sasa amekufa. Nilipigwa risasi na kupenya sehemu ya juu ya sikio langu la kulia. Nilijua mara moja kuwa kuna kitu kibaya kwa kuwa nilisikia sauti ya kishindo, milio na risasi. mara akahisi risasi ikipasua kwenye ngozi.

    "Kutokwa na damu nyingi kulitokea, kwa hivyo nikagundua ni nini kilikuwa kinatokea. Mungu Ibariki Marekani!"

  6. Habari, karibu katika taarifa zetu