Watu 30 wahofiwa kufariki dunia kwa kukanyagana Haiti

Chanzo cha picha, Getty Images
Watu wasiopungua 30 wanahofiwa kufariki dunia kwa kukanyagana katika eneo maarufu la utalii nchini Haiti siku ya Jumamosi.
Tukio hilo lilitokea wakati wa mkusanyiko wa kila mwaka wa Pasaka katika sehemu inayoitwa Citadel ya Laferrière, eneo la urithi wa dunia linalotambulika na UNESCO. Jean Henri Petit, mkuu wa ulinzi wa kiraia katika idara ya Nord nchini Haiti, alisema idadi ya vifo huenda ikaongezeka zaidi.
Waziri Mkuu Alix Didier Fils-Aimé alisema tukio hilo lilitokea “wakati wa tukio la utalii lililohudhuriwa na vijana wengi” katika eneo hilo, katika mji wa kaskazini wa Milot.
Alisema uchunguzi umeanzishwa na “mamlaka zote husika” zimehamasishwa kusaidia walioathirika.
“Serikali inatoa pole za dhati kwa familia zilizoathirika,” Fils-Aimé alisema katika taarifa.
Eneo hilo lilikuwa limejaa wanafunzi na wageni baada ya tukio hilo la uzinduzi wa ngome hiyo ya karne ya 19.
Inaelezwa kuwa mkanyagano huo ulianza karibu na lango la kuingilia eneo hilo na ukachangiwa zaidi na kuanza kwa mvua kubwa.




