Moja kwa moja, Iran yashambulia kambi za kijeshi za Marekani Kuwait

Kumekuwa na ripoti za mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani za Iran kwenye kambi za Marekani huko Kuwait

Muhtasari

Moja kwa moja

Abdalla Seif Dzungu

  1. IG wa Kenya akanusha kuhusika kwa polisi katika utekaji nyara wa mhariri wa kampuni ya Standard

    .

    Chanzo cha picha, NPS

    Maelezo ya picha, Inspekta Jenerali wa Polisi Kenya Douglas Kanja

    Huduma ya Kitaifa ya Polisi nchini Kenya (NPS) imekana kuhusika na kutekwa nyara kwa Mhariri msaidizi wa Standard Group Alex Kiprotich, ikisema imeanzisha uchunguzi ili kubaini utambulisho wa watu wenye silaha waliomkamata kando ya Barabara ya Gilgil Kwenda Nakuru.

    Katika taarifa iliyotolewa Jumatano, msemaji wa NPS Muchiri Nyaga amesema Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja alikuwa ameagiza Kitengo cha Kupambana na Utekaji nyara kuchunguza tukio hilo mara moja, ikiwa ni pamoja na utambulisho wa watu wenye silaha nzito wanaoonekana wakiwaamuru wasafiri kutoka kwenye gari la Kiprotich.

    "NPS inachukulia utekaji nyara kwa uzito mkubwa, kwani makosa haya makubwa yanatishia maisha, uhuru na usalama wa Wakenya," Nyaga alisema.

  2. Ruto aagiza msako dhidi ya wachuuzi wa kigeni ili kuwalinda wafanyabiashara wa ndani

    .

    Chanzo cha picha, State House

    Maelezo ya picha, Rais William Ruto

    Rais William Ruto amewaamuru raia wa kigeni wanaojihusisha na shughuli za uuzaji wa bidhaa za biashara ndogo ndogo nchini Kenya kuacha, akisema serikali itachukua hatua ya kuwalinda wafanyabiashara wa ndani kutokana na ushindani usio wa haki.

    Akizungumza baada ya kukutana na wafanyabiashara wa Biashara ndogo, ndogo na za Kati (MSME) katika Ikulu ya Nairobi, Jumatano, Septemba 2, Ruto alirejelea wasiwasi ulioibuka kwamba baadhi ya wageni wameanzisha biashara zinazouza bidhaa kama vile duvet na bidhaa zingine, wakishindana moja kwa moja na wachuuzi wa ndani na wafanyabiashara wadogo.

    Rais alisema Muswada uliopo mbele ya Bunge hivi sasa unalenga kuwazuia raia wa kigeni kujihusisha na shughuli fulani za biashara nchini Kenya.

    Alitoa wito kwa wafanyabiashara na wadau wengine kujadili sheria iliyopendekezwa kabla ya kupitishwa ili kuhakikisha kwamba mianya yoyote inayowaruhusu wageni kujihusisha na biashara za uchuuzi na biashara zingine ndogo ndogo imeziba.

    "Tuna Muswada Bungeni kwamba kuna baadhi ya shughuli za biashara ambazo wageni hawawezi kufanya nchini Kenya. Kwa mujibu wa sheria, nataka mketi chini na wafanyibiashara waangalie kwa sababu hatujapitisha ili tufunge mianya yote ili mtu asitoke China kuja kuwa mchuuzi," Ruto alisema.

    Rais alisema kwamba hata wakati serikali inasubiri Bunge lifikirie na kupitisha sheria iliyopendekezwa, hatua za kiutawala zitachukuliwa kushughulikia raia wa kigeni wanaofanya kazi kama wachuuzi na wafanyabiashara wadogo.

  3. Iran yashambulia kambi za kijeshi za Marekani Kuwait

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Kumekuwa na ripoti za mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani za Iran kwenye kambi za Marekani huko Kuwait

    Saa moja baada ya jeshi la Kuwait kutangaza katika taarifa kwamba mifumo yake ya ulinzi wa anga ilikuwa imeshirikishwa ili kurudisha kutungua mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora yanayotoka Iran, shirika la habari la Tasnim, karibu na Walinzi wa Mapinduzi, liliandika: "Kambi za Marekani huko Kuwait zilishambuliwa na makombora na ndege zisizo na rubani za Iran."

    Shirika la habari halikutoa maelezo zaidi kuhusu tukio hilo, na CENTCOM - Amri Kuu ya jeshi la Marekani - bado haijajibu ripoti hizo.

    Udhibiti mkali katika nchi za Ghuba ya Uajemi umefanya iwe vigumu sana kwa vyombo vya habari kupata ufikiaji wa moja kwa moja kwenye maeneo yaliyoshambuliwa, na Marekani imeweka vikwazo kwenye uchapishaji wa picha za setilaiti za maeneo haya.

    Siku ya Jumatano, Tasnim ilichapisha picha za angani zinazohusishwa na mashambulizi yake ya Jumanne kwenye kambi za Marekani huko Jordan, ikidai kuonyesha athari zilizoachwa na mashambulizi haya.

  4. Trump aweka sura yake katika sarafu ya dola 1 ya Marekani

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Picha ya Donald Trump imeingia kwenye sarafu ya Marekani – ikiwa mara ya kwanza kwa rais aliye hai kuonekana kwenye sarafu ya Marekani katika karne moja.

    Siku ya Jumatano, Kampuni ya Marekani ya Mint ilizindua sarafu ya ukumbusho ya $1 yenye picha ya Trump pamoja na maneno "Kwa Mungu tunamwamini", kusherehekea maadhimisho ya miaka 250 ya Marekani.

    Sarafu ya toleo maalum ina "roho, fahari, na urithi wa taifa linalokaribia maadhimisho yake muhimu", Kampuni ya Marekani ya Mint ilisema.

    Sarafu hizo - zenye bei ya $61 (£45) kwa roll ya 25 na mfuko wa 100 kwa $154.50 - "hazikuwepo kwa sasa" kwenye tovuti ya Kampuni ya Marekani ya Mint ndani ya saa chache baada ya kuanza kuuzwa.

    BBC imewasiliana na Kampuni ya Marekani ya Mint, Hazina na Ikulu kwa maelezo zaidi.

    Sarafu hiyo "imeundwa kusherehekea hatua hii muhimu ya kitaifa" kwa "muundo wa maadhimisho ya kizazi kimoja unaokusudiwa kuwa nyongeza bora kwa sarafu za kisasa," Kampuni ya Marekani ya Mint ilisema.

    Pia zinauzwa katika mashine za kuuza bidhaa katika duka la US Mint huko Washington DC.

    Ingawa sarafu hizo zina rangi ya dhahabu hazina dhahabu yoyote halisi. Kulingana na US Mint, sarafu hizo zinasharikisha 88.5% ya shaba huku asilimia iliosalia ikiundwa na zinki, manganese na nikeli.

  5. Israel yafichua "mipango iliyoandaliwa" ya kuwafukuza Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty

    Waziri wa Ulinzi wa Israeli Yisrael Katz amefichua kwamba Israeli ina mipango tayari ya kuwaondoa Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza, lakini inasubiri Marekani kufikia makubaliano kuhusu wapi Wagaza watahamishiwa.

    Katika mkutano na waandishi wa habari Jumatano, Katz alisema: "Hatimaye hakuna suluhisho halisi kwa Gaza bila uhamiaji huu," akiongeza kuwa serikali ya Israeli "imepanga na iko tayari kuwaondoa, kwa njia ya baharini, kwa njia ya anga, na kwa kila njia inayowezekana."

    Wakati huo huo, Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema kwamba nchi yake haina mpango wa kujiondoa kutoka eneo lolote lililo chini ya udhibiti wa kijeshi katika Ukanda wa Gaza, akisisitiza udhibiti wa Israeli juu ya eneo hilo.

    Netanyahu alitoa matamshi hayo wakati wa ziara yake Jumatano kwa vikosi vya Israeli huko Gaza.

    Hii ilikuwa ziara ya kwanza ya uwanjani ya Netanyahu tangu makubaliano ya kusitisha mapigano yatangazwe Oktoba iliyopita.

  6. Shambulio la Iran dhidi ya meli ya mafuta ya Saudia laua mabaharia wawili wa Ufilipino - Saudia

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Saudi Arabia imelaani kile ilichosema ni shambulio la Iran dhidi ya meli kubwa ya mafuta inayomilikiwa na Saudi Arabia Jumatatu usiku na kuwaua mabaharia wawili wa Ufilipino.

    Kampuni ya kitaifa ya meli ya Saudi Arabia, Bahri, ilithibitisha Jumatano kwamba meli yake ya Sidr "ilihusika katika tukio la utovu wa usalama wakati ikipitia Mlango-Bahari wa Hormuz".

    Sidr ilipigwa na makombora kaskazini mwa rasi ya Musandam ya Oman, kulingana na makampuni ya usalama wa baharini.

    Meli kubwa ya mafuta inayomilikiwa na Korea Kusini, Senegal Prosperity, iliripotiwa kupigwa mashariki mwa Musandam wakati huo huo.

    Iran haijajibu madai ya Saudi Arabia. Lakini ilisema mapema kwamba meli mbili za mafuta zilishika moto baada ya kugonga mabomu zikitumia njia isiyoidhinishwa kupitia mlango-bahari.

    Habari za vifo vya mabaharia hao zilikuja baada ya jeshi la Marekani kutekeleza wimbi la mashambulizi ya angani dhidi ya Iran na vikosi vya Iran kulenga kambi za Marekani katika nchi jirani za Kiarabu kwa makombora na ndege zisizo na rubani katika ufyatulianaji wao mkubwa wa risasi tangu Julai.

    Siku ya Jumatano waziri wa afya wa Iran alisema watu 18 waliuawa na 108 kujeruhiwa katika mashambulizi ya Marekani.

    Iran imeishutumu Marekani kwa "uhalifu wa kivita" kutokana na shambulio liliowaua watu wanne wakiwemo watoto wawili kwenye sherehe ya harusi katika mji wa kusini wa Sirik. Jeshi la Marekani lilisema linachunguza ripoti hizo.

    Taarifa ya kampuni ya meli Bahri ilisema "tukio la usalama" ambalo halijatajwa lililoathiri Sidr lilitokea katika Mlango-Bahari wa Hormuz yapata saa 23:40 kwa saa za huko (19:40 GMT) Jumatatu.

    "Ni kwa huzuni kubwa kwamba Bahri inathibitisha kufariki kwa mabaharia wake wawili wa Ufilipino kutokana na tukio hilo," iliongeza.

    "Kampuni inatoa rambirambi zake za dhati na salamu za rambirambi kwa familia zao, wapendwa wao, na wafanyakazi wenzao wakati huu mgumu."

  7. EU na Nato zaionya Urusi baada ya taifa hilo 'kuanzisha' mgogoro mpya dhidi ya Ujerumani

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Wakuu wa Nato na Tume ya Ulaya wameonya kwamba Urusi inazidisha uchokozi wake na wameapa kuikabili iwapo itaendelea.

    "Shambulio la Leipzig linaashiria uchokozi mpya katika ardhi ya Umoja wa Ulaya unaohusishwa moja kwa moja na Urusi," alisema Rais wa Tume hiyo Ursula von der Leyen, siku moja baada ya Ujerumani kulaumu Urusi kwa shambulio la ndege isiyo na rubani mwezi uliopita kwenye uwanja wa ndege wa Leipzig.

    "Lazima tuchukue hatua na hiyo ina maana kujibu uzembe wa Urusi haraka na kwa njia bora zaidi," von der Leyen alisema.

    Katibu Mkuu wa Nato Mark Rutte amesema muungano mzima, ambao unajumuisha Marekani, unasimama "kwa mshikamano kamili na Ujerumani".

    Urusi imekataa shutuma za Ujerumani kwamba ndege isiyo na rubani iliyobeba vilipuzi ililenga ndege ya mizigo ya Ukraine kwa makusudi mnamo tarehe 4 Agosti.

    Ndege hiyo iliharibiwa na roboti katika uwanja wa ndege wa Leipzig/Halle na ndege ya pili isiyo na rubani inadhaniwa kugongana na ndege nyingine ya mizigo.

    Ndege ya tatu isiyo na rubani iliripotiwa kupatikana siku 10 baadaye katika uwanja wa ndege, ambao ni kitovu muhimu cha Nato na hutumiwa mara kwa mara na ndege ya usafiri ya Antonov ya Ukraine.

    Ni hadi Jumanne ambapo serikali ya Ujerumani ilisema uchunguzi wa polisi na uchunguzi wa kijasusi umethibitisha kwamba Urusi ilihusika na matukio hayo.

    Waziri wa mambo ya ndani alisema kwamba umbo la ndege isiyo na rubani, vipengele vyake, vilipuzi na kifyatulio chake , vyote vilijulikana kutoka Urusi.

  8. Natumai hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja