Rais wa Israel asema ufyatuaji risasi ni “shambulio la kikatili dhidi ya Wayahudi”

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Israel, Isaac Herzog, ametoa tamko kufuatia tukio la ufyatuaji risasi lililotokea Bondi Australia , akilieleza kuwa ni “shambulio la kikatili sana dhidi ya Wayahudi.”
Inafahamika kuwa wakati tukio hilo linatokea, kulikuwa na hafla ya kuadhimisha siku ya kwanza ya sikukuu ya Kiyahudi ya Hanukkah katika ufukwe wa Bondi.
Hadi sasa, haijabainika wazi nia ya washambuliaji.
“Dada na kaka zetu huko Sydney wameshambuliwa na magaidi waovu katika shambulio la kikatili sana dhidi ya Wayahudi waliokuwa wamekusanyika kuwasha mshumaa wa kwanza wa Hanukkah katika ufukwe wa Bondi,” amesema Herzog.





