Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Hamas yasema mazungumzo mapya ya Gaza yameanza, saa chache baada ya Israel kuanzisha mashambulizi

Hamas inasema wapatanishi wake wamefungua duru mpya ya mazungumzo yenye lengo la kumaliza vita huko Gaza, saa chache baada ya Israel kuanzisha mashambulizi makubwa.

Muhtasari

Moja kwa moja

Lizzy Masinga

  1. Hamas yasema mazungumzo mapya ya Gaza yameanza, saa chache baada ya Israel kuanzisha mashambulizi

    Hamas inasema wapatanishi wake wamefungua duru mpya ya mazungumzo yenye lengo la kumaliza vita huko Gaza, saa chache baada ya Israel kuanzisha mashambulizi makubwa.

    Taher al-Nounou, mshauri wa mkuu wa Hamas, aliambia BBC kuwa duru mpya ya mazungumzo imeanza rasmi mjini Doha siku ya Jumamosi.

    Hakukuwa na masharti kutoka upande wowote, na masuala yote yalikuwa kwenye meza kwa ajili ya majadiliano.

    Israel Katz, waziri wa ulinzi wa Israel, alisema wapatanishi wa Hamas wanarejea katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja nchini Qatar kutafuta makubaliano kuhusu mateka.

    Ilikuja baada ya jeshi la Israeli kusema kwenye akaunti yake ya Kiebrania X kwamba wanajeshi walikuwa wamehamasishwa kwa "Operesheni ya Magari ya Gideoni" ili kuteka "maeneo ya kimkakati" ya Gaza na mateka huru.

    Katika machapisho kama hayo kwenye akaunti yake ya X ya lugha ya Kiingereza, ilisema kwamba haitaacha kufanya kazi "mpaka Hamas isiwe tishio tena na mateka wetu wote wawe nyumbani", na kwamba "imepiga shabaha zaidi ya 150 katika Ukanda wa Gaza" katika kipindi cha saa 24.

    Unaweza kusoma;

  2. Israel yaidhinisha mashambulio 'kudhibiti' maeneo ya Gaza

    Jeshi la Israel limetangaza mashambulio makubwa yaliolengwa kuishinda Hamas na kuhakikisha uhuru wa mateka waliosalia Gaza.

    Vikosi vya ulinzi Israel vimesema katika akaunti yao kwenye ukurasa wake wa Ki Hebrew kwenye mtandao wa X kuwa imeshinikiza vikosi kwa operesheni iliopewa jina "Gideon's Chariots" kudhibiti "sehemu muhimu" za ukanda huo.

    Maafisa wa Wizara ya ulinzi na afya zinazoendeshwa na Hamas wanasema mashambulio ya Israeli yamesababisha vifo vya takriban watu 250 tangu alhamisi.

    Israeli imezuia misaada kuingia katika ukanda huo mnamo Machi baada ya kusambaratika kwa makubaliano ya miezi miwili ya kusitisha mapigano.

    Rais wa Marekani Donald Trump, siku ya Ijumaa amesema "watu wengi wanaathirika kwa njaa" Gaza.

    Jeshi la Israeli haikutumia jina la operesheni hiyo katika ujumbe kama huo kwenye ukurasa wake wa kiingereza kwenye mtandao wa X.

    Limesema hautaacha kuendeleza shughuli zake "hadi pale Hamas itasita kuwa tishio na mateka wetu wote wamerudi nyumbani", na kuwa "imelenga zaidi ya maeneo 150 ya magaidi kote katika ukanda wa Gaza" katika saa 24.

    Israel imezidisha mashambulizi yake na kushinikiza vikosi vilivyojihami mpakani licha ya kuongezeka kwa shinikizo la kimataifa kuendeleza mazungumzo ya kusitisha mapigano na kusitisha mkwamo wake.

    Kuidhinishwa kwa operesheni hii kunaashiria kuwa jitihada zote zimeshindikana.

    Unaweza pia kusoma;

  3. CAF kuzindua taji jipya la soka ya mabingwa Afrika

    Shirikisho la soka barani Afrika CAF litazindua taji na utambulisho mpya wa ligi ya mabingwa barani Afrika kuelekea fainali Mei 24.

    CAF imetangaza kuwa itazindua rasmi taji hilo Mei 22 kabla ya fainali hiyo ya ngwe mbili, ya kwanza ikitarajiwa kuchezwa Jumamosi Mei 24 huko Tshwane na ya pili ikitarajiwa Misri Juni mosi.

    Mabingwa wa soka Afrika na klabu mbili zinazoshiriki, Mamelodi Sundowns na Pyramids FC ni miongoni mwa waliotajwa kushirki uzinduzi huo.

    Uzinduzi huu unatajwa kuashiria awamu nyingine mpya nzito kwa vilabu vya soka Afrika wakati shirkisho hilo likiendelea kukweza hadhi ya mashindano hayo.

    Unaweza kusoma;

  4. Sanamu la mkewe Donald Trump latoweka

    "Melania" alionekana katika ukingo wa mto Sava huko Slovenia mnamo Julai 202, miezi minne kabla ya Melania Trump kuondoka katika ikulu ya Marekani kufuatia kumalizika hatamu ya mumewe Donald Trump.

    Sasa miezi minne baada ya Melanija Knavs kurudi katika makao ya White House kufuatia kurudi madarakani kwa Trump, sanamu lake kubwa lililokuwepo katika ukingo wa mto huo wa Sava limetoweka kutoka mji wa Sevnica alikozaliwa huko nchini Slovenia.

    Kilichosalia kwenye sanamu huyo mkubwa wa shaba ni miguu na kigutu cha mti chenye urefu wa mita mbili ambapo sanamu hiyo ilikuwa ikisimama.

    Hii sio mara ya kwanza kwa tukio la aina hii la kumpa Melania Trump heshima lililoishia na mwisho mbaya huko Sevnica. Sanamu ya kwanza ilizinduliwa mnamo Julai 2019.

    Ilichongwa kutokana na mbao moja na fundi wa eneo hilo Ales "Maxi" Zupevc. Ilikaa kwa mwaka mmoja kabla ya mtu asiyejulikana kuamua kuitekeza moto sanamu hiyo.

    Kwa bahati nzuri msanii wa Marekani Brad Downey, aliyemuagiza Maxi kutengeza sanamu hiyo ya mbao, tayari alikuwa ameshatengeza mfano wa sanamu hiyo ambayo iliundwa upya kwa shaba na kuzinduliwa katika eneo lilo hilo.

    Downey alieleza kuwa sanamu hiyo mpya iliundwa kuwa thabiti kwa kutumia shaba ambayo haiwezi kuharibiwa.

    Lakini inavyoonekana imeweza kukatwa miguuni na kuibiwa. Polisi katika eneo hilo wanauchukulia mkasa huo wa kutoweka kwa "Melania" kama "wizi" na wameidhinisha uchunguzi.

    Unaweza kusoma;

  5. Chris Brown arudishwa rumande kufuatia tuhuma za shambulizi

    Muimbaji nyota wa R&B Chris Brown amenyimwa dhamana na mahakama moja Uingereza na kurudishwa rumandi baada ya kufika mbele ya mahakama hiyo kufuatia tuhuma za kutumia chupa kumshambulia mtu katika klabu ya burudani mjini London Uingereza.

    Muimbaji huyo raia wa Marekani alikamatwa katika Hoteli ya Salford's Lowry siku ya Alhamisi na baadaye akashtakiwa kwa kutuhumiwa kwa shambulio hilo linalosemekana kutokea katika klabu ya Tape mnamo 2023.

    Brown, mwenye umri wa miaka 36, anatuhumiwa kumshambulia na kumuumiza kwa chupa muandaaji muziki Abe Diaw.

    Msanii huyo alikuwa mjini Manchester kuelekea tamasha lake Uingereza lililopangiwa kufanyika Juni na Julai, mjini Manchester na Cardiff.

    Unaweza kusoma;

  6. Watu tisa wauawa kwa shambulizi la ndege zisizo na rubani la Urusi nchini Ukraine

    Watu tisa wameuawa katika shambulizi la ndege zisizo na rubani za Urusi dhidi ya basi la abiria kaskazini-mashariki mwa Ukraine, maafisa wa eneo hilo wamesema.

    Utawala wa eneo la Sumy unasema watu wengine wanne walijeruhiwa katika mji wa Bilopillia Jumamosi asubuhi.

    Madaktari, wafanyakazi wa huduma za dharura na polisi sasa wanafanya kazi katika eneo la tukio.

    Shambulio hilo limeripotiwa saa chache baada ya Urusi na Ukraine kufanya mazungumzo yao ya kwanza ya moja kwa moja ya amani tangu 2022.

  7. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu leo