Serikali tupunguze matumizi makubwa ya mafuta- Rais Samia

Chanzo cha picha, Standard NP
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameelezea athari ya vita vya Iran kwa dunia nzima ikiwemo Tanzania, hususan katika kupanda kwa bei ya mafuta na upungufu wa mafuta.
Aidha amesema kutangazwa kusitishwa kwa vita hivyo na kufunguliwa kwa mlango bahari wa Hormuz ni jambo la faraja.
''Hii inatupa matumaini makubwa sana kama serikali na ile kuruhusu tu meli za awali za Ufaransa,za Japan.....kidogo nimeona bei ya mafuta imeshuka kidogo sasa hii inatupa matumaini.'' Alisema.
Lakini hata hivyo, amechukua hatua pia kupunguza matumizi makubwa ya mafuta yaliyopo serikalini kwa kuanzia kwanza na ofisi yake.
"Ndani ya serikali tuna matumizi makubwa ya mafuta, magari ni mengi, safari zetu ni nyingi niwaombe sana tuanze kupunguza matumizi ya mafuta, kwa kuanza na ofisini kwangu ninapotembea kuanzia sasa wote nitawaingiza kwenye kibasi''.
Aidha amesema upandaji wa bei ya mafuta umekuwa ukienda sambamba na kupanda kwa bei za bidhaa, hivyo amewataka wananchi kuwa watulivu.
Maelezo zaidi:


















