Mwanamke wa Marekani ambaye alimshutumu Rais wa Marekani Joe Biden kwa kumnyanyasa kingono amesafiri kwa ndege hadi Moscow na anatafuta uraia wa Urusi.
Akizungumza na chombo cha habari cha serikali ya Urusi, Tara Reade, 59, alisema anajisikia salama nchini humo na alitaka kubaki huko.
Bi Reade alidai Bw Biden alimshambulia alipokuwa akifanya kazi katika ofisi yake ya bunge mwaka wa 1993.
Alikanusha vikali madai yake."Haijawahi kutokea, haijawahi kutokea," alisema.
Bi Reade alifanya kazi kama msaidizi wa Bw Biden alipokuwa seneta wa Delaware.
Aligonga vichwa vya habari mnamo 2020 wakati kampeni yake ya urais ilipokuwa ikiendelea, alipodai kwamba alimshambulia huko Capitol Hill alipokuwa na umri wa miaka 29.
Alimshutumu kwa kumsukuma ukutani na kuweka mikono yake chini ya shati na sketi yake.
"Niliposhuka kwenye ndege huko Moscow, kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu sana nilijihisi salama, na nilihisi kusikika na kuheshimiwa," gazeti la The Guardian linamnukuu Bi Reade akisema wakati wa mahojiano na Sputnik.
Alisema aliondoka Marekani baada ya mwanasiasa wa chama cha Republican kumwambia kuwa maisha yake yalikuwa hatarini.
"[Ningependa] kutuma maombi ya uraia wa Urusi, kutoka kwa rais wa Shirikisho la Urusi, Vladimir Putin... Ninaahidi kuwa raia mwema," Bi Reade alisema, na kuongeza kuwa anatumai kutunza uraia wake wa Marekani. .
Bi Reade alikuwa mmoja wa wanawake kadhaa waliojitokeza mnamo 2019 na 2020 kumshutumu Bw Biden kwa kuguswa vibaya, kukumbatiana au kupigwa busu.Alisema alikuwa amewasilisha malalamiko, ingawa hakuna rekodi yoyote iliyopatikana na haijulikani ikiwa madai yake yalichunguzwa rasmi.
Msemaji wa Bw Biden alisema anaamini kuwa wanawake "wana haki ya kusikilizwa" lakini tukio hilo linalodaiwa "halikutokea kabisa".