Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tabu Mtingita: Mwanangu husema mama mi naona aibu unavyochekesha
Katika umri wa miaka 41, Nyota ya @tabumtingita kutoka Tanzania inaonesha nuru katika Sanaa ya uchekeshaji, Licha ya kukabiliana na maoni ya manyanyaso na matusi katika mitandao ya kijamii Tabu hajakata tamaa kuendelea na talanta yake ya uchekeshaji.
Mwandishi wa BBC veronica Mapunda amezungumza na Bi Tabu kujua namna anavyokabiliana na changamoto hizi na jinsi anavyomudu majukumu ya kuwa mama wa mtoto ambaye hafurahii kazi afanyayo mama yake?