Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rais Samia azitaka Tanzania, Uganda ziondoe vikwazo vya biashara
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewataka mawaziri wanaohusika na masuala ya biashara na uwekezaji wa Tanzania na Uganda wakutane haraka kwenye tume ya pamoja ya ushirikiano waangalie changamoto zilizoainishwa kwenye kongamano la wafanyabiashara ili ziondoshwe.
Hayo yamesemwa leo na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan aliposhirikiana na mwenzake wa Uganda, Yoweri Museveni katika kongamano la wafanyabiashara wa Tanzania na Uganda jijini Dar es Salaam,akizitaka pande mbili ziondoe kero zinazokwamisha ushirikiano wa kibiashara.