Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Virusi vya corona: 'Hatuna nafasi ya kuichoma miili', raia wa India waeleza
Idadi ya vifo kutokana na janga la corona imeongezeka kwa kiasi kikubwa nchini India, kukiwa na upungufu wa dawa na oksijeni.
Familia zimekuwa zikisubiri kwa saa nyingi-siku kadhaa- kufanya taratibu zao za mwisho za kuchoma miili ya wapendwa wao kutokana na ukosefu wa nafasi kwa ajili ya shughuli hiyo.
Jumatatu India ilirekodi maambukizi makubwa kwa siku ikiwa ni siku ya tano mfululizo na kufika idadi ya watu 352,991 na imeendelea kushuhudia idadi hiyo ikiongezeka kila siku.