Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Godbless Lema: Akamatwa Kenya kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria
Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Kaskazini mwa Tanzania Godbless Lema anashikiliwa nchini Kenya baada ya kudaiwa kuingia nchini humo kinyume na taratibu.
Kwa mujibu wa wakili wake, Lema ambaye alikua ameambatana na familia yake alikua akielekea jijini Nairobi kwa ajili ya kutafuta makaazi ya muda.
Hata hivyo amesema kushikiliwa huko hakuhusiani kwa vyovyote vile na masuala ya kisiasa.