Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uchaguzi Tanzania 2020: Mkurugenzi wa uchaguzi Zanzibar azungumzia madai ya changamoto ya vitambulisho vya mpigakura
Taifa la Tanzania linatazamiwa kufanya uchaguzi wake mkuu wenye kuhusisha madiwani, wabunge na rais ifikapo October 28 Mwaka huu.
Ni uchaguzi wa Tanzania bara na visiwani. Hata hivyo kila mpiga kura atatakiwa kuwa na kitambulisho ili kumuwezesha kushiri haki yake ya kimsingi ya kupiga kura.
Lakini visiwani Zanzibar, suala la vitambulisho vya mpiga kura limekua tata.
Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar Thabit Faina Amezungumza na mwandishi wetu Aboubakar Famau, na kwanza amemuuliza kuhusu malalamiko ya baadhi ya wananchi kwamba mpaka sasa hawajapata vitambulisho hivyo.