Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wakristo wanaolazimika kuadhimisha Krismasi msituni
Wakristo wa Jimbo la Aceh, Indonesia wanaadhimisha Krismasi kwenye mahema katikati ya msitu.
Makanisa yao yalishambuliwa na kuvunjwa mwaka 2015 na makundi ya waislamu na mamlaka za eneo hilo. Mamlaka hizo pia zinadai wakristo hao hawana kibali cha kujenga upya nyumba zao za ibada.
Indonesia ndiyo taifa lenye idadi kubwa zaidi ya Waislamu duniani, taifa hilo lina katiba inayoruhusu uwepo wa dini mbalimbali. Lakini hata hivyo, stahmilivu na masikilizano ya kidini yamekuwa ni ya kuzorota katika miaka ya hivi karibuni.