Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Enzi ya Mugabe madarakani
Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amefariki dunia akiwa na miaka 95 nchini Singapore.
Mugabe amekuwa kiongozi wa Zimbabwe toka 1980 mpaka 2017. Alikuwa Waziri Mkuu hadi 1987 alipochukua usukani kama rais wa nchi hiyo, na mwishowe kung'olewa kwa msaada wa jeshi.
Utawala wake awali ulisifiwa kwa kuinua maisha ya raia na kukuza uchumi lakini mwishowe ulishutumiwa kwa ukandamizaji wa upinzani, ukiukaji wa sheria za uchaguzi, na kusababisha uchumi wa nchi kuanguka.