Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tete Kafunja: Umuhimu wa adhabu ya kifo kuondolewa Tanzania
Tete Kafunja alikwenda kutoa dhamana kwa rafiki yake aliyekamatwa kwa kosa la kuuza bangi, baada ya kufika hapo alikamatwa na kupewa kesi ya mauaji.
Kabla ya hapo Tete alikua akiendesha biashara ya kuuza vinywaji vya pombe maarufu kama Bar maeneo ya Manzese Jijini Dar Es salaam. Alikua na mke na mtoto mmoja.
Baada ya kukamatwa alikaa gereza la keko jijini Dar es salaam kwa miaka 11 kama mahabusu akisubiri hukumu yake.