Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Shule inayotoza karo kupitia taka za plastiki
Akshar Forum katika Jimbo la Assam Mashariki mwa India imebuni njia ya kipekee ya wanafunzi kulipa karo ya shule. Wanahitajika kupeleka taka za plastiki kila wiki. Mradi huo ulianza kutekelezwa mwezi Oktoba mwaka 2018 baada ya waanzilishi wake kugundua kuwa plastiki zinachomwa nje ya nyumba zao. Kampeni hiyo ya kulinda mazingira ni moja ya miradi inayoendeshwa katika shule hiyo ambapo wanafunzi wanapewa elimu ya kawaida na mafunzo ya ziada itakayowawezesha kujitegemea baada ya kukamilisha masomo yao ya msingi.