Jivunie Mbunda anazungumzia kukataliwa kwasababu ya ulemavu Tanzania

Maelezo ya video, Jivunie Mbunda anazungumzia kukataliwa kwasababu ya ulemavu Tanzania

Jivunie Mbunda ni mwanamume mwenye ulemavu Tanzania. Amemuoa Bahati Ramadhani tangu Mei mwaka huu. Hatahivyo kabla ya kupata upendo na furaha hii - anakiri haikuwa rahisi kwani aliwahi kukataliwa zaidi ya mara kumi kutokana na ulemavu wake. Anazungumzia changamoto za mlemavu kukubalika katika jamii Tanzania alipokutana na mwandishi wa BBC Eagan Salla.