Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Vijana wa Kenya waliozuru Urusi kutazama kombe la Dunia wazungumza
Kundi moja la vijana kutoka eneo la Marsabit nchini Kenya limewasili kutoka Urusi ambapo lilikuwa limeenda kutazama mechi kati ya Uhispania dhidi ya Urusi. Mpango huo unatokana na shirika moja la kijamii kwa jina HODI ambalo linawashawishi vijana mjini Marsabit kucheza soka kwa lengo la kuleta amani na mshikamo katika kaunti hiyo huku likiwasaidia wasichana wadogo kukwepa ukeketaji . Walituelezea kuhusu ziara hiyo ya Urusi na umuhimu wake.