Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wafungwa Kenya wafunzwa yoga kuwapunguzia mawazo
Je umeshawahi kufikiria jinsi watu walioko magerezani wanavyoishi siku baada ya siku bila uhuru wa kufanya lolote na mahangaiko tele ya mawazo kuhusu maisha yao na jamii walizoziacha nyumbani?
Wanahabari wa BBC Anythony Irungu na Anne Ngugi walizuru gereza la wanawake la Machakos na kushuhudia wafungwa wakifanyishwa mazoezi kupitia wa mazoezi ya maungo, kutafakari na kudhibiti pumzi maarufu kama yoga.
Mazoezi hayo huwasaidia wafungwa kusukuma siku gerezani na angalau wapate lepe la usingizi.