Panya wavamia mtambo wa ATM na 'kutafuna' pesa nchini India

Chanzo cha picha, Getty Images
Mafundi waliofika kuukarabati mtambo wa ATM ambao ulikuwa umeharibika katika jimbo moja nchini India walipigwa na butwaa walipoufungua kubaini tatizo lilikuwa wapi.
Noti za thamani ya rupia 1.2m (£13,300; $17,600) zilikuwa zimechanwa na kuraruliwa na panya katika benki hiyo jimbo la Assam.
Polisi wanasema panya hao pengine waliiingia ndani ya mtambo huo kwa kupitia kwenye tundu lililokuwa litumiwe kuingizia nyaya, gazeti la Hindustan Times limeripoti.
Picha zinazoonesha pesa zilizokuwa zimetafunwa na panya hao katika mtambo huo wa Benki ya Dola ya India katika wilaya ya Tinsukia zimesambazwa sana kwenye Twitter.
Moja inaonesha mzoga wa mmoja wa panya hao kwenye mabaki ya noti hizo.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Afisa wa polisi Prakash Sonowal alisema kwamba mtambo huo umekuwa haufanyi kazi kwa siku 12 hizi, gazeti la Hindustan Times limeongeza.
Mafundi waliofungua mtambo huo walipata noti za rupia 2,000 na rupia 500 zikiwa zimeharibiwa.
Walifanikiwa kunusuru noti za jumla ya thamani ya rupia 1.7 milioni, maafisa wanasema.

Unaweza kusoma pia:













