Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Paul Ogalo: Kasisi anayetumia nyimbo za kufoka kuwavutia vijana Kenya
Kasisi mmoja wa kanisa Katoliki nchini Kenya Paul Ogalo a.ka ‘Sweet Paul’ anatumia muziki wa kufoka kama njia ya kuwavutia vijana kufika kanisani.
Anasema aliona muziki kuwa njia mwafaka sio tu kuwavutia vijana bali pia kueneza Injili.
Kwa sasa anaandaa albamu mpya ya muziki wa kufoka na ana matumaini ya kufanya kazi na wasanii wa Kenya na Tanzania akiwemo Bahati, Wyre na Nameless na nyota wa muziki kutoka Tanzania Diamond.
Video: Anthony Irungu, BBC