Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanawake Kenya waandamana kwa hasira kushinikiza haki ya mama kumyonyesha mwana
Wanawake wameandamana leo Nairobi kulalamika kufukuzwa kwa mama aliyemnyonyesha mwanawe katika mgahawa mmoja mjini. Taarifa hiyo imezusha hisia kali kote nchini na kusababisha makundi ya kutetea haki za wanawake kuandaa maandamano ya leo mjini. Dhamira kuu ni kushinikiza haki za akina mama waungwe mkono na kusaidiwa katika kufanikisha kuwanyonyesha watoto wao bila ya ubaguzi wa aina yoyote.