Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
George Weah: Mchezaji nyota alivyoibuka na kuwa rais wa Liberia
Mchezaji wa zamani wa klabu za Monaco, AC Milan na Chelsea George Weah ameapishwa kuwa rais wa Liberia, na kuchukua uongozi kutoka kwa Ellen Johnson Sirleaf ambaye amestaafu.
George Weah alianza maisha yake mtaa wa mabanda lakini akang’aa sana kama mchezaji na kuwa Mwafrika wa pekee kushinda tuzo ya Ballon d’Or.
Ilikuwaje hadi mwanamume huyo anayefahamika sana kama Mfalme George Liberia akawa rais wa taifa hilo la Afrika Magharibi?